• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wafanyabiashara wahimizwa kushirikiana na Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: January 16th, 2020

WAFANYABIASHARA wa Soko la Matunda, Samaki wabichi na mbogamboga la Bonanza katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kushirikiana na Jiji la Dodoma na pia kuacha kufanya biashara kwa mazoea, badala yake waboreshe ili waweze kufikia malengo na kujiinua kiuchumi.

Aidha, wametakiwa kutumia fursa za ukuaji wa kasi wa Jiji la Dodoma na ongezeko kubwa la idadi ya wakazi kulikosababishwa na uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma.  Hivi sasa kuna idadi kubwa ya watu wanaoweza kununua bidhaa zao mbalimbali.

Ushauri huo ulitolewa na Mwenyekiti wa soko hilo, Marwa Mabucha, wakati akizungumza na wafanyabiashara baada ya kuchaguliwa kwenye uchaguzi mkuu wa viongozi wa soko hilo uliofanyika jijini Dodoma.

Vilevile, aliwataka wafanyabiashara hao kuachana na biashara za mazoea ambazo hazina tija, badala yake wafanye kwa malengo ya kuinua mitaji yao ili waweze kupata mikopo ambayo itawawezesha kukabiliana na wingi wa wateja wanaowahudumia.

Mabucha alisema bila wafanyabiashara kubadilisha mtizamo wao wa kizamani wa kufanya biashara kimazoea kwa idadi ile ile ya watu wakati ikiwa Manispaa hawataweza kujiinua kiuchumi na kuendana na mahitaji ya sasa katika Jiji la Dodoma.

Mwenyekiti huyo ambaye alichaguliwa kwa kura 196, aliwataka wafanyabiashara hao kushirikiana kwa pamoja na Halmashauri ya Jiji ili kuweza kuboresha soko hilo kwenye miundombinu.

Kwa upande wake mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Goya Magwai, aliutaka uongozi uliochaguliwa kushirikiana na wafanyabiashara hao pamoja na Jiji ili waweze kuwahudumia wateja wao na kutatua changamoto zilizopo.

Katika uchaguzi huo viongozi wengine waliochaguliwa ni pamoja na Makamu Mwenyekiti Fortunatus Keleta, aliyechaguliwa kwa kura (119), Katibu wa soko Dickson Mwesigwa (209), Katibu Msaidizi Hamisi Mbula (105) na Mtunza Hazina Elias Manikulu (286).

Chanzo:www.ippmedia.com

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.