• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapitisha Bajeti 2025/2026 shilingi bil. 147

Imewekwa tarehe: January 31st, 2025

Na. Coletha Charles, DODOMA

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lapitisha kwa kauli moja rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 jumla ya shilingi bilioni 147.9 ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.04 ukilinganisha na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2024/2025.

Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri wa jiji hilo, ambao ulilenga kupitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026.

Akiwasilisha rasimu hiyo, Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda, alisema kuwa halmashauri imekasimia kukusanya shilingi bilioni 67.3 kati ya fedha hizo bilioni 43 ni mapato yasiyolindwa na shilingi 24.3 ni mapato lindwa, ambapo halmashauri ipo kwenye kundi ambalo asilimia 70 ya mapato yasiyolindwa inayoelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 30 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Alisema kuwa, rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 itagharamiwa na vyanzo vikuu vinne ikiwemo serikali kuu shilingi bilioni 68.9 kati ya fedha hizo shilingi 68.8 (Mishahara na Matumizi ya kawaida) na shilingi Bilioni 10 ni ununuzi wa vifaa tiba na dawa, Halmashauri ya Jiji kupitia mapato ya ndani shilingi bilioni 67.3, wahisani shilingi bilioni 11.7 na ubia (PPP) ambapo mwaka wa fedha 2025/2026, Halmashauri inategemea kuanza ujenzi wa Miradi mikubwa ambayo tayari ilishafanyiwa usanifu na upembuzi yakinifu. “Kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji, naomba kuwasilisha rasimu ya makisio ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Jiji ya Dodoma kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 kuwa ni jumla ya shilingi bilioni 147.9, kati ya fedha hizo shilingi bilioni 67.3 ni mapato ya ndani, shilingi bilioni 65.7 ruzuku ya mishahara, shilingi bilioni tatu (3) ruzuku ya matumizi mengineyo na shilingi bilioni 11.7 ruzuku ya miradi ya maendeleo” alisema Kaunda.

Akichangia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti hiyo, Diwani wa Kata ya Viwandani, Jaffari Mwanyemba, alisema kuwa bajeti hiyo ni kubwa ambayo itafanikisha miradi yote kutekelezwa na kuleta maendeleo. Alishauri kuwa serikali iangalie kwa ukubwa eneo la stendi ya zamani ya daladala, Jamatini kwa kufanyia maboresho kuepuka maswali kipindi cha uchaguzi. “Bajeti ambayo imekuja mahali ambapo tunaihitaji na wananchi wetu wanahitaji matokeo mazuri. Mama Samia mwaka 2024/2025 ametutendea haki ametupatia fedha zaidi ya vile ambavyo tulitarajia hakika yote aliyofanya ni utekelezaji wa ilani yetu ya Chama Cha Mapinduzi. Kwahiyo, mwezi wa kumi tunakazi ya kufanya ili kuleta matokeo chanya.” alisema Mwanyemba.

Nae, Diwani wa Viti Maalum Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Anna Mng’ong’o, alisema kuwa bajeti ya mwaka huu inaenda kujibu na kumaliza matatizo yote katika kata kulingana na fedha iliyotengwa. “Huu mwaka ni mwaka wa uchaguzi, bajeti ni nzuri na imekidhi na tunaenda kwa wananchi kujibu maswali kifua mbele kwa sababu tutakuwa tumefanya mambo mazuri, tunampongeza mkurugenzi na jopo lake kwakweli wamefanya jambo zuri sana” alisema Mng’ong’o.

 

Ikumbukwe kuwa, katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026, mambo mapya yatakayofanyika ni pamoja na utekelezaji wa mradi wa kuongeza mnyororo wa thamani kwa mazao ya zabibu na mboga mboga ambapo itahususha mashamba, ujenzi wa kiwanda cha kuchakata zabibu eneo la Nala, kujenga ‘Park House’ kwa ajili ya kuhifadhia zao la mbogamboga, ambapo kwa kiasi kikubwa itapunguza changamoto ya soko la zabibu na wananchi watapata fursa ya kuuza mbogamboga kwenye masoko ya ndani na nje ambapo kazi ya upembuzi yakinifu imeshaanza na inafanywa na TAHA (Tanzania Holticuture Association) na uanzishaji wa mji wa kisasa Hombolo Bwawani ambao utaunganishwa na mji wa Serikali Mtumba.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.