• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapitisha rasimu ya Sheria ndogo tano

Imewekwa tarehe: March 30th, 2025

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

NAIBU Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago amesema kuwa mchakato wa kuandaa Sheria ndogo za halmashauri yake ilizingatia miongozo inayoelekeza uandaaji wa sheria hizo kwa maslahi ya wananchi wa Dodoma.

Alitoa kauli hiyo katika Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupitia rasimu za Sheria ndogo za Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. 

Naibu Meya Chibago alisema kuwa baraza lake limejiridhisha kuwa kila hatua imepitiwa vizuri ya mchakato wa kuandaa Sheria ndogo za halmashauri. Mchakato ulikuwa shirikishi na ulianzia hatua za mwanzo kwa mujibu wa miongozo. Kamati za Maendeleo za Kata hadi vikao vya juu vya halmashauri. “Tumejadiliana kwa kina na kuheshimu maoni ya kila mtu. Nawahakikishia kuwa yale tuliyojadili leo, vielelezo vyote vipo kwa mujibu wa miongozo kutokana na umakini wa baraza hili” alisema Chibago.

Awali akiwasilisha Rasimu ya Sheria ndogo za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Wakili Cosmas Nsemwa alisema kuwa serikali za mitaa zimepewa mamlaka ya kutunga Sheria ndogo chini ya kifungu cha 88 cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura ya 288. “Utaratibu wa kutunga Sheria ndogo kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma umeainishwa kwenye kanuni ya 75 ya kanuni za kudumu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Tangazo la Serikali Na. 478 la tarehe 1 Julai, 2022” alisema Wakili Nsemwa.

Aidha, alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inakusudia kutunga Sheria ndogo tano kwa ajili ya udhibiti wa shughuli mbalimbali pamoja na kuanzisha vyanzo vipya vya mapato. “Rasimu zote za Sheria ndogo zimeandaliwa kwa kuzingatia mambo yafuatayo;- Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Sura 290 Kifungu 16 (1) Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Sura ya 288 Kifungu cha 88,89 na 90. Mwongozo wa Uandishi wa Sheria ndogo wa Mwaka 2022 uliotolewa na Mwandishi Mkuu wa Sheria, Kanuni ya 75 ya Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma Tangazo la Serikali Na. 478 la tarehe 1 Julai, 2022, mapendekezo ya idara tumizi, maoni ya Kamati ya Maendeleo ya Kata (WDC), kata zote na maoni ya wadau mbalimbali” alisema Wakili Nsemwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri aliipongeza halmashauri kwa kuandaa rasimu ya Sheria ndogo vizuri. “Moja ya mambo ya msingi kuacha alama ni kutungwa kwa Sheria ndogo ili mapato ya serikali yapatikane. Baraza lazima kujihoji mara mbili kwa nini kuanzisha Sheria ndogo hizi” alisema Shekimweri.

Aidha, alielezea sababu za kushindwa kutekelezeka kwa Sheria ndogo kuwa ni uzembe wa kuzisimamia Sheria hizo. “Kama kusipokuwepo na uwezeshwaji vitendea kazi na rasilimali fedha, mfumo wa ufuatiliaji, elimu na uhamasishaji wananchi kuzingatia Sheria ndogo, hizi sheria hazitatekelezeka na itakuwa kazi bure kuandaa mipango isiyotekelezeka” alisema. 

Sheria ndogo tano zilizopitishwa na Mkutano wa Baraza la madiwani ni Sheria Ndogo ya (Ada na Ushuru) ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mwaka 2024; Sheria Ndogo ya (Ushuru wa Madini ya Ujenzi) ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mwaka 2024; Sheria Ndogo ya (Ushuru wa Usimamizi na Uendeshaji wa Masoko), Minada na Magulio) ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mwaka 2024; Sheria Ndogo ya (Maegesho na Udhibiti wa Vyombo vya Usafiri) ya Halmashauri ya Jiji ya Mwaka 2024; Sheria Ndogo ya (Ada na vibali vya shughuli za kiutamaduni) ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mwaka 2024

 


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.