• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Bodaboda wamchangia Rais Samia 3,170,000/= za kuchukua fomu ya kugombea Urais mwaka 2025

Imewekwa tarehe: July 8th, 2024

Na. James K. Mwanamyoto OR-TAMISEMI

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa amepokea mchango wa shilingi 3,170,000/= wa madereva bodaboda nchini, walioutoa kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa ajili ya kumuwezesha kuchua fomu ya kugombea urais mwaka 2025 baada ya kuridhishwa na uongozi wake.

Mhe. Mchengerwa amepokea mchango huo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salam, wakati akizindua sare maalum (uniform) na mfumo wa kidijitali (kanzidata) wa madereva Bodaboda na bajaji wa jiji la Dar es Salaam.

“Leo nimeshuhudia na kupokea mchango wenu wa kumuwezesha Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuchukua fomu ya kugombea urais mwaka 2025 kwa mapenzi yenu wenyewe, bila kushurutishwa na hii ni kwasababu Rais Samia ameingia katika mioyo yenu na watanzania wengine kutokana na uongozi wake imara,” Mhe. Mchengerwa ameeleza.

Mhe. Mchengerwa amesema, uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan umegusa mioyo ya madereva boda boda, wakulima, wafanyakazi na kila mtanzania, hivyo kila mmoja kwa nafasi yake ana sababu ya kumuunga mkono kwa vitendo kwa kumchangia ili aweze kutimiza azma yake ya kuendelea kuliongoza taifa na kuliletea maendeleo.

Waziri Mchengerwa amewapongeza viongozi wa boda boda kutoka katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Tanga, Mwanza, Geita, Katavi, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa, Lindi,Tabora, Dar es Salaam pamoja na Zanzibar kwa kuwasilisha michango yao ya kumuwezesha Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuchukua fomu ya kuombea urais mwaka 2025.

“Fedha hizi 3,170,000/= mlizo changa na kunikabidhi, nami leo hii hii nitakwenda kuzikabidhi kwa Mhe. Rais ili atambue namna ambavyo mna muunga mkono kutokana na kuthamini uongozi wake madhubuti na imara,” Mhe. Mchengera amesema.

Waziri Mchengerwa ameahidi kuwa, Serikali itaendelea kuthamini mchango wa madereva boda boda na bajaji wanaoutoa katika maendeleo ya taifa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.