• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC SHEKIMWERI: “Tufuate Utaratibu Mzuri wa Tume Huru ya Taifa Uchaguzi ili tulinde Jiji la Dodoma”

Imewekwa tarehe: March 22nd, 2025

Na. Leah Mabalwe, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, awataka viongozi wa vyama vya siasa pamoja na wananchi kufuata maelekezo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kutovuruga maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

 Aliyasema hayo katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Dodoma kilichoketi kujadili taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini na kuzalisha Jimbo la Mtumba pamoja na Jimbo la Dodoma mjini. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji.

“Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatoa fedha nyingi kwaajili ya kuboresha Mji wa Dodoma. Hivyo, napenda kuwaomba sana viongozi wangu mbalimbali wa vyama vya siasa pamoja na vijana wote kwa ujumla kuelekea katika uchaguzi mkuu wa serikali, kufuata taratibu nzuri na kuepuka vurugu, na ili kuepuka vurugu ni kufuata utaratibu mzuri wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuanzia wakati wa kujiandikisha pamoja na kuboresha taarifa katika daftari la kudumu la mpiga kura. Hivyo, inakupa haki ya kwanza ya kupiga kura kwa kujisifu kwa kuwa na kadi ya kupiga kura” alisema Alhaj Shekimweri.

Pia aliongezea kwa kuwasisitizia viongozi wote wa vyama vya siasa kutoa elimu kwa wananchi juu ya kutunza amani na umuhimu wa kupiga kura. “Kila kiongozi wa chama cha siasa anawajibu wa kutoa elimu kwa wananchi ili kulinda amani pamoja na kujitokeza katika kupiga kura. Hivyo, kila kiongozi anawajibu mkubwa sana wa kuwapa elimu wananchi wake. Nina imani kuwa haya mambo yote yakifuatwa hakutatokea na tatizo lolote la kuvuruga amani. Nawaomba sana kufuata utaratibu mzuri uliowekwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi’’ alisisitiza Alhaj Shekimweri. 

 


Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Hazina, Tunu Mahmoud, alipongeza zoezi hilo la ugawaji majimbo kwasababu fursa zitaongezeka na kuweka mipaka ya utawala mzuri kwa watendaji wa umma pia itarahisisha upatikanaji na utoaji wa huduma kwa ukaribu. 

“Zoezi hili la ugawaji wa majimbo kati ya Jimbo la Mtumba pamoja na Jimbo la Dodoma Mjini kwa upande wangu ni jambo zuri hii itasaidia upatikanaji wa huduma wa karibu na haraka kwa wananchi. Pia itaongeza fursa za kijamii na kiuchumi pamoja na kuweka mipaka mizuri kwa watumishi wa umma. Hivyo ni jambo zuri na jiji letu la Dodoma litazidi kukua na kupata maendeleo zaidi” alisema Mahmoud.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.