• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Diwani Makole asema neno kwa Machinga Dodoma

Imewekwa tarehe: March 1st, 2025

Na. Shahanazi Subeti, MAKOLE

Diwani wa kata ya Makole, Halmashauri ya Jiji la Dodoma Omary Haji amewapongeza wafanyabiashara wadogo wadogo (Machinga) wa Mkoa wa Dodoma kwa kuwa na umoja na mshikamano katika utendaji wa kazi kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

Aliyasema hayo wakati wa makabidhiano rasmi ya Ofisi ya Viongozi wa Machinga Mkoa wa Dodoma iliyojengwa Kata ya Makole ambayo imegharimu shilingi milioni 56 zikiwa ni jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa Machinga katika taifa. 

Haji alisema “nawashukuru sana Machinga wa Mkoa wa Dodoma, wakiongozwa na wenyeviti wao na viongozi wengine kwa kuweza kuungana katika kufanikisha ujenzi wa ofisi hii na kwakuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kuwatambua Machinga wa Dodoma na kuwajengea ofisi katika eneo hili linaweza kuwasaidia na kuwarahisishia shughuli zenu za kibiashara. Kwahiyo, ni wazi kabisa mtalitunza na kulithamini vizuri jengo hili”.

Sambamba na hilo alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa utu na kuthamini wafanyabiashara wadogo wadogo (Machinga) kwa kufanya mapinduzi katika Kata ya Makole. “Kwahiyo, nina imani kabisa mtalienzi vizuri jengo hili na kama mnavyoliona jengo ni la kisasa zaidi na mmewekewa 'furniture' nzuri lakini mmependezeshewa na jengo lenu ni zuri kuliko hata ofisi ya kata” alisema Haji.

Pia aliongezea kwa kuwataka Machinga kuweza kuwa makini na miundombinu ya ofisi ili iendelee kuwa imara zaidi. “Leo tunaikabidhi ofisi hii, ambayo ndani imekamilika kila kitu, sasa ni jukumu lenu kuweza kusimamia vizuri kwa umakini na kuweza kuhakikisha kwamba vitu vyote  vilivyopo hapa vipo salama. Lakini kutunza mazingira ya eneo lenu la kazi kwa kupanda miti, nina imani kabisa kwa umoja wenu hili jengo linaenda kuwa jipya siku zote. Pia muweze kushirikiana na wenzenu ambao wapo hapa, kuwepo kwenu kwenye Kata ya Makole kunaweza kuchangia haswa maendeleo katika soko letu” alisema Haji.

Mkuu wa Divsheni ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Charity Sichona, alielezea kuwa ujenzi wa Ofisi ya Machinga Mkoa wa Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa agizo kwa serikali kwamba kila mkoa kujenga ofisi kwa ajili ya viongozi wa Machinga kwa lengo la kurahisisha utoaji huduma kwa wafanyabiashara hao. “Kwahiyo, mara ya kwanza alitoa shilingi milioni 10 kwa kila mkoa kwa kuanza ujenzi. Baada ya ile shilingi milioni 10 kukamilisha ujenzi wake, Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliongezea shilingi milioni 26.2 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi. Hadi kufikia hatua ya kukamilika kwa jengo hili jumla ya shilingi milioni 56 zimetumika” alisema Sichona.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.