• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt. Msonde awataka walimu kuleta Mapinduzi katika Elimu

Imewekwa tarehe: March 3rd, 2024

Na. James Mwanamyoto, OR-TAMISEMI

NAIBU Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Elimu) Dkt. Charles Msonde amewataka walimu wote nchini kuhakikisha wanaleta mapinduzi katika elimu kwani Serikali inawatengemea katika eneo hilo na ndio kipaumbele kimojawapo cha Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Msonde ametoa wito huo kwa walimu , kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na walimu wa Halmashauri za Wilaya ya Gairo, Kilosa na Mvomero ambao wanahudhuria mafunzo ya walimu wa masomo ya sayansi na kiingereza kwa shule za msingi kupitia siku maalumu ya MEWAKA nchini.

“Mwalimu ukiamua unaweza kufanya mambo makubwa sana katika taifa letu na ndio maana Serikali ya Awamu ya Sita inawategemea katika kuleta mapinduzi ya elimu ambayo ni mojawapo ya kipaumbele cha Mheshimiwa Rais,” Dkt. Msonde amesisitiza.

Dkt. Msonde amesema, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka watoto wa kitanzania wapate ujuzi unaostahili, na kuongeza kuwa Mhe. Rais anatarajia wanafunzi wote wa darasa la kwanza, la pili na la tatu wajue kusoma na kuandika kwa ufasaha.

Dkt. Msonde amesema kuwa, walimu wakiwafundisha vizuri watoto ni dhahiri kuwa watapata umahiri wa kusoma, kuandika na kuhesabu ikiwa ni pamoja na umahiri wa masomo yote wanayofundishwa.

“Mnapofundisha lengo lisiwe kumaliza kurasa za vitabu bali mjikite katika kuhakikisha watoto wanapata ujuzi katika somo husika na umahiri ndio jambo la kupewa kipaumbele,” amesema Dkt. Msonde.

Dkt. Msonde ameeleza bayana kuwa, Serikali inawaamini na kuwathamini walimu wote nchini na ndio maana inajali maslahi yao hivyo ni jukumu lao kuamua kutekeleza wajibu wao kikamilifu kwa mustakabali wa elimu na masilahi mapana ya taifa.

Jumla ya walimu 60,036 nchini wanahudhuria mafunzo ya walimu wa masomo ya sayansi na kiingereza kwa shule za msingi kupitia siku maalumu ya MEWAKA kupitia vituo mbalimbali vilivyopo katika wilaya zao.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.