• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DUWASA watatua kero ya maji Nzuguni

Imewekwa tarehe: October 10th, 2022

NAIBU Waziri wa Kilimo na Mbunge Dodoma wa Mjini, Anthony Mavunde, ameipongeza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa kuweza kushirikiana na wananchi katika kutatua kero ya maji licha ya changamoto zote zilizopo.

Ameyasema hayo leo tarehe 10 Oktoba, 2022 wakati wa ziara yake katika eneo la Nzuguni ambapo visima vitano vimechimbwa katika eneo hilo.

“Ninampongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutatua changamoto ya upungufu wa maji katika jiji la Dodoma, tunamshukuru Rais kwa mipango ya muda mrefu ya kati na mipango ya muda mfupi ya kutatua changamoto hii.” Alisema Mavunde.

Alisema yeye kama Mbunge ataendelea kuishauri serikali namna nzuri ya kupata maji kabla ya utekelezaji wa miradi mikubwa kuanza na kuweka fedha katika uchimbaji wa visima virefu pembezoni ili tuweze kupata maji ya uhakika.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa majisafi Nzuguni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa DUWASA, Mhandisi Aron Joseph alisema zaidi ya wakazi 37,000 waishio katika ukanda wa Nzuguni jijini Dodoma wanatarajia kunufaika na mradi wa maji baada ya kubainika uwepo wa bonde lenye maji mengi katika eneo la hilo.

“Maeneo ambayo utafiti na uchimbaji visima unaendelea yanamilikiwa na wananchi na mara baada ya kukamilika kazi hizo zoezi la uthamini litafanyika kwa ajili ya kulipa fidia ili kuyatwaa kwa matumizi ya mamlaka.”

Alibainisha kuwa mradi huo utaongeza uzalishaji wa majisafi kutoka wastani wa lita milioni 67.8 hadi lita milioni 75.5 kwa siku sawa na ongezeko la asilimia 11.4 ya uzalishaji wa sasa.

“Ongezeko hili litaongeza asilimia 11.7 ya mahitaji ya sasa ya jiji lote la Dodoma ambayo ni lita milioni 133.8 kwa siku,”alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini, Mhe. Jabir Shekimweri aliipongeza DUWASA kwa hatua hiyo huku akiishauri kuendelea na kasi ili kupata maji maeneo mengine.

Aidha, alishauri wananchi wanaopisha miradi hiyo kulipwa fedha zao mapema ili eneo libaki kuwa chanzo cha maji na wanaojenga wajulishwe kuhusu kuzingatia suala la upandaji miti ili kutunza mazingira.

Pia, aliishauri DUWASA kuzingatia afya ya walaji kwa kuhakikisha mkondo wa maji hauingiliani na mfumo wa majitaka.

Chanzo: duwasatz (instagram)

Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mhe. Anthony Mavunde akionja maji kutoka kwenye kisima kipya eneo la Nzuguni Jijini Dodoma leo.

Mhe. Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde (wa nne kushoto mbele) akiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma (mwenye suti na tai) pamoja na viongozi wengine walipotembelea mradi wa uchimbaji visima katika eneo la Nzuguni Jijini Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.