• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

EWURA yakabidhi msaada wa mashuka 431 kwa Vituo vya Afya Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: June 23rd, 2021

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji (EWURA), imetoa msaada wa mashuka 431 kwa Vituo vya afya vinne vilivyo chini ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Msaada huo wenye thamani ya shilingi 5,000,000 (Milioni tano) umetolewa ili kusaidia uboreshaji wa huduma za afya katika Jiji la Dodoma ambalo linakabiliwa na ongezeko la idadi ya watu.

Akitoa msaada huo leo tarehe 23 Juni 2021 Jijini Dodoma, Kaimu Mkurugenzi wa EWURA, Mhandisi Godfrey Chibulunje amesema kuwa wametoa msaada huo ili kuongeza kasi ya utoaji huduma bora za afya kwa wananchi katika vituo vya afya vya Makole, Mkonze, Hombolo na Kikombo.

Mhandisi Chibulunje amesema kuwa msaada huo wameutoa ikiwa ni mchango wa EWURA kwa jamii hususani katika kipindi hiki cha kuhitimisha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini.

Amefafanua kuwa msaada huo utagawiwa katika vituo vya afya vilivyolengwa kwa kuzingatia mahitaji halisi katika kila kituo.

"Tumetoa msaada wa mashuka 431 kwa Jiji la Dodoma na yataenda kwa vituo vya afya vinne vya Makole, Hombolo, Mkonze na Kikombo, tumechagua mwaka huu kusaidia eneo la afya na mwaka mwingine tutaangalia eneo lingine", amesema Mhandisi Chibulunje.

Aidha, katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma, mamlaka hiyo imetoa mafunzo kwa watumishi wake na kutembelea watoa huduma mbalimbali wanaowasimamia lengo ikiwa ni kubaini changamoto wanazokabiliana nazo ili waweze kuzitatua.

"Lengo leru ni kuhakikisha mlaji anapata huduma bora kwa viwango vinavyosimamiwa na mamlaka yeru." Amefafanua zaidi Mhandisi Chibulunje.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method amesema kuwa Jiji la Dodoma linatoa shukurani  kwa msaada huo wa kusaidia jamii kwenye sekta ya afya.

Dkt. Method amesema kuwa kwa wastani katika Kituo cha Afya Makole, wajawazito 120 hujifungua kila wiki, hivyo kwa mwezi idadi ya wajawazito wanaojifungua katika kituo jicho hufikia kati ya wajawazito 400 hadi 600. 

"Tutahakikisha msaada huu unatumika katika maeneo yaliyokusudiwa, na tunaishukuru sana EWURA kwa kuwa mstari wa mbele kusaidia sekta ya afya, ikumbukwe kuwa EWURA walishatoa msaada wa vifaa vya kutunza watoto wanaozaliwa wakiwa njiti." Amesema Dkt. Method.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.