• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

GIZ yaipa Wizara ya Afya vifaa vya TEHAMA vya Milioni 300

Imewekwa tarehe: August 27th, 2021

WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea msaada wa vifaa vyenye thamani ya shilingi Milioni 300 kutoka Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika la GIZ kwa ajili ya kuboresha huduma za Afya nchini, ikiwemo kupunguza vifo vya mama na mtoto kupitia mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Akipokea vifaa hivyo leo jijini Dodoma, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Abel Makubi amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Serikali ya Ujerumani katika kuboresha Sekta ya Afya hususan katika kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuboresha huduma ya Bima ya Afya, mifumo ya TEHAMA na ukarabati wa miundombinu.

"Wajerumani wamekuwa marafiki zetu, na wamekuwa wakitusaidia katika maeneo mbali mbali, sio tu katika Sekta ya Afya peke yake bali katika Sekta nyingine. Katika Sekta ya Afya wamekuwa wakisaidia kwenye kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuboresha huduma ya Bima ya Afya, mifumo ya TEHAMA na ukarabati wa miundombinu ambapo wamejikita katika Mikoa ya Tanga na Mbeya." Amesema.

Prof. Makubi amesema Shirika hilo la GIZ na KFW katika kipindi cha miaka 60 limejikita katika kusaidiana na Serikali kutoa huduma kwa wananchi katika mikoa ya Tanga na Mbeya ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa kuboresha huduma za mama na mtoto, kuboresha huduma kupitia mifumo ya TEHAMA na suala la uongozi.

Aidha, Prof Makubi amesema kuwa, Serikali ya Ujerumani kupitia GIZ itaendelea kusaidia Tanzania katika kusimika mifumo ya ‘GOTHOMIS’ hasa katika ngazi ya Halmashauri na kuachana na mfumo wa makaratasi katika katika utoaji wa huduma na utunzaji wa kumbukumbu hali itayosaidia kuboresha huduma kwa wananchi, ikiwemo ukusanyaji wa mapato.

Naye Meneja Mradi kutoka Shirika la GIZ Bw. Erick Msofe amepongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuboresha Sekta ya Afya, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika maboresho hayo ikiwemo vita dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19.

Vifaa vilivyopokelewa na Wizara ya afya ni pamoja na Kompyuta Mpakato (laptops) pamoja na Kompyuta za mezani (Desktops) jumla zikiwa 119.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.