• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kuhudumia Majimbo Mawili ya Uchaguzi

Imewekwa tarehe: March 22nd, 2025

Na. Faraja Mbise, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga vema kutoa huduma kwa wananchi wote kwa kuzingatia mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini wenye mapendekezo ya kuligawa jimbo hilo kuwa Jimbo la Mtumba lenye jumla ya kata 20 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye kata 21.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, mara baada ya majadiliano kutoka kwa Madiwani kuhusu taarifa iliyowasilishwa na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga ya kuwasilisha mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani  katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. 

Dkt. Sagamiko alisema “mgawanyo huu kwa sasa unalenga mgawanyo wa jimbo kuwa majimbo mawili, bado tutaendelea kuwa na halmashauri moja kwa maana ya utoaji huduma kwa ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Jiji litaendelea kuwajibika katika utoaji wa huduma katika majimbo yote mawili”.

Akizungumzia kuhusu mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, alisisitiza kuwa, mgawanyo huo utazingatia zaidi kata na sio tarafa. “Kwa minajili ya jambo letu la leo la kupendekeza mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, tutaangalia zaidi kata na wakati utakapofika kutoa mapendekezo ya mgawanyo wa tarafa na mtaa kwa mamlaka zile basi tutarejea tena katika utaratibu wa kawaida” alisisitiza Dkt. Sagamiko.


Sambamba na hilo, alitoa rai kuwa, baraza lijikite katika mipaka ambayo inatambulika kwa mujibu wa sheria “nilikuwa nashauri baraza lako lijikite katika mipaka ambayo kwa sasa inatambulika kwa mujibu wa sheria, kwamba tunazo kata 41 na mitaa 222. Hivyo, vingine kwa sasa bado hatuna. Kwahiyo, mipango yetu yote nashauri tuweze kujikita hapo na pale itakapopendeza taratibu nyingine zitaweza kufuatwa” alishauri Dkt. Sagamiko. 

Mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini umezingatia hali ya kiuchumi ya jimbo hasa suala la ukusanyaji mapato, lengo ikiwa ni kuona maeneo yaliyopo juu kiuchumi hayamezi kiuwakilishi maeneo yaliyo chini kiuchumi.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.