• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

JIJI LA DODOMA LAIBUKA KINARA MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2023

Imewekwa tarehe: November 28th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma limeibuka kinara katika mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 iliibuka nafasi ya kwanza kimkoa, kikanda na nafasi ya pili kitaifa.

Taarifa hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akitoa maelezo mafupi kuhusu matokeo ya mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 katika kikao cha mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya na watendaji katika mkoa na halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Senyamule alisema kuwa mwaka 2023 Mkoa wa Dodoma ulikuwa mkoa wa 30 kabla ya mkoa wa kilele kukimbiza Mwenge wa Uhuru. “Wakimbiza Mwenge wa Uhuru wanakuwa na vigezo wanavyoangalia hasa wanaangalia fedha zilizoletwa zimetumikaje, ubora wa miradi iliyoletewa fedha na Mheshimiwa Rais imesimamiwaje kwa tija na ufanisi kiasi gani na kuona jinsi ambavyo tumehamasisha wananchi kupokea ujumbe wa Mwenge wa Uhuru ambao ni ujumbe wa kitaifa kwa lengo la kuongeza umoja na mshikamano kitaifa” alisema Senyamule.

Alisema kuwa mkoa ulipokea barua kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Vijana, Kazi na watu wenye Ulemavu ikionesha matokeo ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 kwa kila halmashauri, kimkoa, kikanda na kitaifa.

“Niseme mambo machache katika Mkoa wa Dodoma halmashauri tano zimeingia katika 10 bora. Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeshika nafasi ya kwanza kimkoa, nafasi ya kwanza kikanda na nafasi ya pili kitaifa” alisema mkuu wa mkoa.

Halmashauri nyingine zilizoingia 10 bora ni Halmashauri ya Mji Kondoa imeshika nafasi ya pili kimkoa, nafasi ya pili kikanda na nafasi ya sita kitaifa. “Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa imeshika nafasi ya tatu kimkoa, nafasi ya tatu kikanda na nafasi ya nane kitaifa. Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na Kongwa zimefungana zikiwa nafasi ya nne kimkoa, nafasi ya nne kikanda na nafasi ya 10 kitaifa” alisema Senyamule huku akibubujikwa na tabasamu la wazi.

Alisema kuwa matokeo hayo yamepelekea Mkoa wa Dodoma kufikia asilimia 83.54 ya ufanisi kwenye shughuli za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023. “Dodoma mwaka 2022 tulishika nafasi ya 22 kitaifa jambo hilo halikutufurahisha, tulipeana shime kuwa hiyo siyo nafasi yetu kama mkoa. Kutokana na matokeo hayo na juhudi mbalimbali zilizofanyika mwaka huu kwa mara ya kwanza katika historia ya Mkoa wa Dodoma, Mkoa wa Dodoma umeshika nafasi ya kwanza kitaifa” alisema Senyamule kwa furaha.

Ikumbukwe kuwa kikao cha mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya na watendaji katika mkoa na halmashauri kiliongozwa na mkuu wa mkoa, kikihudhuriwa na Kamati ya Usalama Mkoa, Katibu Tawala Mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa, waratibu wa Mwenge wa Uhuru na maafisa wengine waandamizi wa serikali.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.