• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Halmashauri zapewa wiki mbili kutambua majengo, mabango ya kodi

Imewekwa tarehe: February 9th, 2021

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewapa wiki mbili Viongozi wa Sekretarieti za Mikoa, na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha kuwa ndani ya wiki mbili kuanzia sasa wawe wamesimika mfumo wa kutambua orodha ya majengo na mabango yaliyopo katika maeneo yao ili kurahisisha ukusanyaji wa kodi na ushuru.

Akizungumza wakati wa kikao kilicho wakutanisha, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini jana  jijini Dodoma, Mhe. Jafo amesema, changamoto kubwa ambayo inasababisha zoezi la ukusanyaji kodi za majengo ni kutokuwepo kwa orodha kamili ya majengo katika mamlaka husika.

Waziri Jafo alisema suluhu ya kudumu itakayosaidia kuyabaini kwa wepesi na kurahisisha ukusanyaji wa kodi za majengo na ushuru wa mabango ni kuwepo kwa mfumo utakaosaidia kuyabaini majengo yote na mabango na kuhifadhi kumbukumbu hizo katika Kompyuta.

“Tunataka kuanzia tarehe 05 hadi 28 Februari, 2021, iwe ni kazi ya kubainisha majengo yote yanayopaswa na ambayo yanakidhi kulipiwa kodi,” amesema Waziri Jafo na kuongeza kuwa nyumba za matope zimeondolewa katika utaratibu huu.

“Kila Mtendaji wa Mtaa, Mwenyekiti wa Kijiji anatakiwa kuwa na takwimu za majengo yote yanayopaswa kulipiwa kodi, Mkurugenzi hakikisha kuwa Mtendaji wako wa Kijiji au Mtaa anakupatia takwimu ndani ya Wiki mbili kuanzia leo,” alisisitiza Mhe. Jafo.

Waziri Jafo amesema, Wakurugenzi wa Halmashauri watatakiwa kuwasilisha kanzi data hizo ngazi ya Wilaya kwa ajili ya uhakiki kwa Mkuu wa Wilaya, kabla ya kuwasilisha ngazi ya Mkoa kwa Katibu Tawala wa Mkoa na ifikapo tarehe 04 Machi, 2021 zoezi hilo liwe limekamilika na taarifa ya majumuisho iwe imetumwa kwa Katibu Mkuu TAMISEMI.

Waziri amesisitiza kuwa, taarifa hizo zitatakiwa kuanisha nyumba, mmiliki na mawasiliano yake kwa wepesi wa rejea, ambapo mara baada ya hapo, itafanyika kampeni maalum ya kuanza kukusanya kodi ya majengo nchi nzima, itakayoanza tarehe 22 Machi hadi tarehe 05 Aprili, 2021.

“Tunataka huko mbeleni hizi Mamlaka za Serikali za Mitaa ziweze kufanya baadhi ya shughuli za Maendeleo zenyewe, hivyo katika zoezi hili tutaweka mfumo maalum utakaoweza kuona mambo kadhaa yanayo endelea nchi nzima kwenye kazi hii, hatutaki watu washindane bali tunataka kila Halmashauri iwe ya kwanza,” amesema Mhe. Jafo.

Kuhusu vitambaulisho vya wajasiriamali, Waziri Jafo, amesema tayari vitambulisho million 1.6 vimechapishwa na mamlaka ya Mapato Tanzania na kusambazwa katika Mikoa.

“Huu ndio mwanzo na maelekezo ya Serikali, ambayo yatakuwa katika makundi matatu, Wafanya Biashara wakubwa wanaolipa kodi TRA, Wafanyabishara wa kati wenye Leseni za Halmashauri na kundi la tatu ni wenye Vitambulisho vya Mjasiriamali, kila mmoja wetu lazima awe sehemu ya kundi moja wapo” amesema Waziri Jafo

Amesema kuwa asiyekuwa na kitambulisho au hana kundi lolote kati ya hayo, asiruhusiwe kufanya biashara.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Aldolf Ndunguru amesema pamoja na kwamba zoezi la kukusanya kodi hizo limehamishiwa Mamlaka za Serikali za Mitaa bado anaamini ushirikishwaji madhubuti wa viongozi katika maeneo mbali mbali utawezesha kukabiliana na mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali.

Akitoa salamu za Mamlaka ya Mapato nchini, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA, Dkt Edwin Mhede, ametaka kuwepo ushirikiano na Wakuu wa Wilaya kwani maeneo hasa ya upande wa forodha bado hali siyo nzuri kama matarajio na malengo yao yalivyo, hivyo akaomba msaada wa karibu kutoka kwa viongozi hao ambao ni wenyeviti wa Kamati za ulinzi za Wilaya.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.