• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lapokea bilioni 3, kuzalisha viwanja 700

Imewekwa tarehe: November 9th, 2021

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepokea mkopo wa fedha Shilingi Bilioni 3 kutoka Serikali Kuu kupitia utekelezaji wa programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha ardhi nchini ambapo fedha hizo zitatumika kutwaa maeneo yatakayopimwa na kuzalisha viwanja 700 vya ukubwa na matumizi mbalimbali.

Mgao huo ulitangazwa jana Novemba 8, 2021 na mawaziri watatu akiwemo Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi na Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Ummy Mwalimu.

Akizungumza jijini Dodoma wakati wa hafla ya utiaji saini ya makubaliano wa utoaji wa fedha za mikopo ya utekelezaji wa programu ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi nchini, Waziri Nchemba amezitaka Halmashauri hizo kuzitumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa.

Nchemba amezitaka Halmashauri 55 zilizopokea mikopo ya fedha yenye thamani ya shilingi bilioni 50 kuhakikisha wanazitumia vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa na kuzirudisha kwa wakati ili Halmashauri zingine zipate fursa za kukopa. "Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 50 kwa halmashauri 55 nchini kupitia wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili kusaidia upimaji wa ardhi kwenye maeneo yao. Lengo la Serikali kutoa mikopo hiyo ni kuziwezesha halmashauri hizo kupima ardhi na kuondoa ujenzi wa holela kwenye maeneo hayo." Alisema Nchemba. 

Aliendelea kusema kuwa “Serikali itaendelea kutoa fedha hizo kutokana na hali ya bajeti itakavyokuwa imepangwa, hivyo waliopata mikopo hiyo wanatakiwa kuonyesha mfano kwa wengine watakaohitaji,” alisema.

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeeo ya Makazi, William Lukuvi alisema kupitia fedha hizo Halmashauri zitaweza kutengeneza Bilioni 41 huku akitolea mfano Halmashauri ya Meru imekopa shilingi bilioni 1.6 na inatarajia kuingiza shilingi bilioni 7.8.

Waziri Lukuvi alisema siku za nyuma Halmashauri zilikuwa zikiomba mikopo kutoka taasisi za kifedha lakini awamu hii serikali imechuku jukumu hilo. Mikopo hiyo imetolewa na serikali kutokana na andiko lililoandikwa na halmashauri husika kuhusu kazi za fedha hizo. Waziri Lukuvi alisema kuwa jumla ya halmashauri 78 ziliomba mikopo hiyo lakini waliofanikiwa ni halmashauri hizo 55 na watakuwa wakitoa mikopo hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha.

Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Ummy Mwalimu aliagiza mapato ya ndani ya maendeleo katika Halmashauri kutumika pia katika kupima na kupanga miji bila kutaja asilimia ambazo zinatakiwa kutengwa. Hatua hiyo ilikuja kufuatia Waziri Lukuvi kumuomba Waziri Ummy kuwa Halmashuri zitenge fedha kidogo kwa ajili ya kupima na kupanga maeneo.

Waziri Ummy alisema kupatikana kwa fedha hizo imeongeza vipaumbele alivyokusudia kwenye utendaji wake wa kazi alivyojiwekea wakati anaingi kwenye wizara hiyo. Amevitaja vipaumbele hivyo kuwa ni huduma za afya, elimu msingi, kuwawezesha wananchi kiuchumi hasa akina mama, walemavu na vijana, na ujenzi wa miundombinu ya barabara. Waziri Mwalimu alisema kwa sasa ameongezewa kipaumbele cha tano kuwa ni upimaji ardhi kwenye halmashauri mbalimbali nchini. Aidha, alisema kuwa “Upatikanaji wa fedha hizo utachochea ukuaji wa uchumi kwa wanachi pamoja na halmashauri husika,”



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.