• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kamati ya Usalama Wilaya ya Dodoma yawahakikishia wananchi hakuna tukio la uvunjifu wa amani

Imewekwa tarehe: July 5th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Usalama ya Wilaya ya Dodoma imewahakikisha wananchi wa Mtaa wa Kizota Relini kuwa hakuna tukio lolote la uvunjifu wa amani litakaloruhusiwa kutokea katika eneo hilo kufuatia mgogoro wa ardhi uliodumu zaidi ya miaka 10.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Wilaya ya Dodoma, Godwin Gondwe alipokuwa akiongea na waandishi wa habari baada ya kikao cha ndani na viongozi wa wananchi wa eneo la Muhuji katika Mtaa wa Kizota Relini jijini hapa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Gondwe ambae ni Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Dodoma alisema “niwahakikishie wananchi wa eneo la Muhuji katika Mtaa wa Kizota Relini kuwa kuna usalama wa kutosha katika eneo hilo. Hakuna mwananchi atakayesumbuliwa kwa namna yoyote. Dodoma ni salama na ina amani na waandishi wa habari mnafahamu serikali ipo macho na haitakubali kuona mtu yeyote anayewakosesha amani wananchi”.

Akiongelea utatuzi wa mgogoro wa ardhi katika eneo hilo, alisema kuwa uongozi wa wilaya na halmashauri una jukumu la kutatua migogoro ya ardhi. “Leo tupo hapa kwa ajili ya kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 10. Tumekutana na makundi yote yanayohusika na mgogoro huu. 

Tumetengeneza timu ya wananchi watano waliopendekezwa na wananchi wenyewe ili kuweza kuutatua. Tumekaa hapa na Mstahiki Meya Prof. Davis Mwamfupe na Mkurugenzi wa Jiji John Kayombo. Tumetoa siku saba kufuatilia historia ya mgogoro huu na kuutatua. 

Kundi la kwanza tutakutana nalo kesho saa 2 asubuhi na kundi la pili tutakutana nalo saa 5 asubuhi. Jiji la Dodoma hatutaki kuzalisha migogoro ya ardhi, muelekeo wa Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais ni kumaliza migogoro ya ardhi Dodoma.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Makazi katika eneo la Muhuji, Simba Shaban alisema “nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuwaona ninyi na kuwateua kuja kumsaidia ndani ya Wilaya ya Dodoma. Niwapongeze kwa moyo wa utashi na ubinadamu wa kutusikiliza”.

Wananchi wa eneo la Muhuji katika Mtaa wa Kizota Relini walikumbwa na taharuki baada ya kuona askari wakitekeleza majukumu yao ya kulinda amani katika eneo hilo kufuatilia mgogoro wa ardhi uliodumu zaidi ya miaka 10.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.