• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kanisa la Anglikana latakiwa kulinda maadili na kukemea maovu kwa vijana

Imewekwa tarehe: August 15th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amelitaka Kanisa la Anglikana kulinda maadili na kukemea maovu kwa vijana ili wawe raia wema katika jamii.

Kauli hiyo aiitoa alipokuwa mgeni rasmi katika tukio la ufunguzi wa jengo la kitega uchumi (Safina house) la Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika, tukio lililofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu jijini hapa.

Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisema “nihimize kulinda maadili na kukemea maovu katika jamii kwa vijana. Lakini wapo wakubwa wanaolitumia kanisa kufanya maovu, kemeaneni”.

Aidha, Rais alilipongeza kanisa hilo kwa ujenzi wa jengo la kitega uchumi (Safina house). “Jengo hili limebadilisha na kuleta mandhari ya kupendeza kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Hii ni hatua moja ya kujitegemea kwa Dayosisi ya Central Tanganyika. Huduma zilizosubiriwa kwa miaka sita zimeanza kupatikana. Nimefurahi kuona nembo ya NMB hapa. Serikali imefurahishwa na kukamilika kwa mradi huu kwa sababu utachangia katika ukuaji wa uchumi na jamii” alisema Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akitoa maelezo ya Askofu na kumkaribisha mgeni rasmi, Askofu wa Dayosisi ya Central Tanganyika, Mhashamu Dkt. Dickson Chilongani alisema kuwa jengo la kitega uchumi lilianza kujengwa mwaka 2017. Jengo hilo liligharimu shilingi bilioni nane. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni mbili ni msaada kutoka marafiki wa Marekani, shilingi bilioni tatu ni jitihada za ndani na shilingi bilioni tatu ni mkopo kutoka benki.

Kuhusu usanifu wa jengo hilo, alisema kuwa sura ya jengo la Safina ni ukumbusho wa Mungu kutumia Safina kumuokoa Nuhu na familia yake. “Jengo la Safina litumike kuleta wokovu kwa wakazi wa Jiji la Dodoma na viunga vyake” alisema Mhashamu Dkt. Chilongani.

Kwa upande wa salamu za Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alisema kuwa Mkoa wa Dodoma upo salama na wananchi wanaendelea na shughuli za kujiletea maendeleo.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa Mkoa wa Dodoma umeanza kupokea wanafunzi wa kidato cha tano mwaka 2023 na wanafunzi wote wanapata sehemu za kulala. Alisema kuwa jumla ya shule 10 mpya zinajengwa katika Mkoa wa Dodoma za kuanzia kidato cha kwanza hadi kidato cha nne.

Akiongelea utekelezaji wa miradi mikubwa, aliitaja kuwa mradi wa maji wa shilingi bilioni tano unaojengwa katika eneo za Nzuguni unatarajia kuongeza upatikanaji wa maji kutoka 50% hadi 67%. Mradi wa Barabara ya Mzuguko, ujenzi wake umefikia 40%. Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato umefikia 20% na ujenzi wa Mji wa Serikali Mtumba umefikia 62.5%. “Mheshimiwa Rais, Mkoa wa Dodoma tunatoa pongezi kwa vipaumbele vyako vinavyogusa maisha ya watu wa kawaida” alisema Senyamule.

 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.