• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Kata ya Mkonze yabainisha watoto wenye mahitaji maalum kupata elimu

Imewekwa tarehe: January 10th, 2025

Na. Coletha Charles, MKONZE

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea na zoezi la kubainisha watoto wenye mahitaji maalum kwa lengo la kujiunga na elimu ya awali na msingi kwa mwaka 2025, kwa ushirikiano na viongozi wa kata, mitaa na wazazi.

Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Afisa Mtendaji wa Kata ya Mkonze, Herieth Reuben, alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum kupata fursa za kielimu na kijamii zinazolingana na mahitaji yao. 

Alisema kuwa kata hiyo ina wakazi 41,000, mitaa nane na shule 12 za msingi. Hivyo, wamejipanga kusimamia shughuli ya uandikishaji kwa asilimia 100 na watapita kila kaya kuwabainisha watoto wenye mahitaji maalum ili waweze kuanza masomo yao. “Hii ni sehemu ya mpango wetu wa kuhakikisha kuwa watoto wote wanapata haki zao za msingi bila ubaguzi, tunaomba wazazi watupe ushirikiano ili tuweze kuboresha maswala ya elimu. Lakini pia watoto wengi wenye mahitaji maalum watapata huduma stahiki, watajiunga na elimu ya msingi kwa sababu kata yetu tumewaandikisha na tunaendelea kuwaandikisha” alisema Reuben.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mkonze, Saidi Waziri, alitoa pendekezo kwa Jiji la Dodoma kuweza kuwahamasisha wazazi kuwapeleka watoto wenye mahitaji maalum shule kwa kutoa taarifa kupitia makanisa na misikiti. “Shule yetu ni jumuishi inachukuwa watoto wa kawaida na wenye mahitaji maalum. Hadi sasa tuna watoto wenye uhitaji maalum wapatao 18, ambao wanaendelea kusoma, lakini leo tumeandikisha watoto watatu ambao watajiunga na darasa la kwanza” alisema Mwalimu Waziri.

Nae, Mwenyekiti wa Mtaa wa Chidachi, Kata ya Mkonze, Mohamedi Missanga, alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajengea vyumba vya madarasa 16 kwa muda wa miaka miwili. “Wazazi wapate ushawishi wa kuwapeleka watoto shule na wawalete waandikishwe. Tutahakikisha tunawatafuta na kuwabaini watoto wote wenye mahitaji maalum, nyumba kwa nyumba, tukishirikiana na mbunge, madiwani, viongozi wa mashina na tutawabaini wale wote ambao watakuwa wamewaficha watoto ili serikali ya awamu ya sita iwashughulikie” alisisitiza Missanga.

Kwa ujumla, zoezi hilo limelenga kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata nafasi sawa ya kufikia ndoto zake, huku ikisisitizwa umuhimu wa kuendeleza ushirikiano wa jamii na serikali katika kuwahudumia watoto wenye mahitaji maalum.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.