• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maafisa Waandikishaji Jiji la Dodoma watakiwa kufungua vituo kwa wakati

Imewekwa tarehe: October 11th, 2024

Na. Faraja Mbise, DODOMA

MAAFISA waandikishaji Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameaswa kuzingatia muda wa kufungua na kufunga vituo vya uandikishaji orodha ya wapiga kura unaotarajiwa kufanyika tarehe 11-20 Oktoba, 2024.

Wito huo ulitolewa katika mafunzo kwa maafisa waandikishaji wa Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika ukumbi wa Mtumba Complex tarehe 08 Oktoba, 2024 na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga.

Akizungumza na maafisa waandikishaji orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuzingatia muda wa kufungua  na kufunga vituo vya kujiandikisha wapiga kura ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pindi wawapo katika maeneo yao ya kazi.

“Vituo vyetu kama mlivyotangaziwa vitafunguliwa saa mbili kamili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili jioni. Sasa isije ikatokea ukaona hakuna watu ukaweka vitabu kwenye begi ukaondoka. Sisi tunapita kukagua kila kituo na bahati nzuri kila kata, kila mtaa kuna mtu anayesimamia huo mtaa. Kwahiyo, kuna mtu atakuwa anatembea na bodaboda kukagua wewe utamuona kama muandikishwaji ila yupo” alisema Kasoga.

Aidha, aliwataka maafisa waandikishaji kutambua sifa za mtu anayepaswa kuandikishwa kwenye orodha ya daftari la mpiga kura na sifa za mpiga kura baada ya kuandikishwa.

“Kuna mambo yafuatayo lazima tuyazingatie sana, jambo la kwanza, mtu huyu ni lazima awe raia wa Tanzania, tunapoenda kufanya kazi zetu lazima tuhakikishe kwamba kuwa ni raia wa Tanzania, endapo itatokea utamuandikisha mtu ambae siyo raia wa Tanzania changamoto yake tutakwenda kwenye pingamizi na itakwenda kufanya marekebisho ya orodha ya wapiga kura. Jambo la pili, awe na miaka 18 na zaidi. Jambo la tatu ni lazima awe mkazi wa mtaa husika na lazima awe mtu mwenye akili timamu” alisisitiza Kasoga.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Wakili Cosmas Nsemwa aliwaasa maafisa waandikishaji kutumia lugha nzuri yenye ukarimu pindi watoapo huduma kwa waandikishwaji katika vituo vyao vya kazi. Aliongeza kuwa wasitumie lugha ya matusi ambayo itaweza kupelekea zoezi kuharibika.

“Tuwe na lugha nzuri kwa wananchi wetu wanaokuja kujiandikisha.  Kwahiyo, kutumia hizo lugha zenye matusi na maudhi ukibainika utakuwa umefanya kosa” alisema Wakili Nsemwa.

Aidha, kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Uratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Odero, alitoa maelekezo kuhusu vifaa ambavyo vitatumika wakati wa zoezi la uandikishaji wa orodha ya wapiga kura na kuwataka maafisa waandikishaji kutunza vifaa hivyo kwasababu baada ya zoezi vitahakikiwa baada ya zoezi.

“Unapokabidhiwa vifaa vya umma na mwisho unayomaliza kuvitumia utahakikiwa. Kwahiyo, tutakapowakabidhi vifaa, tutakabidhi kwa nyaraka. Kwahiyo, tunategemea kwamba siku ambayo unakuja kuchukua vifaa, Afisa Mtendaji wa Kata husika na watu wake tutakuwa tunagawa kata kwa kata ambapo tutakuwa tunauwisha nyaraka hizo kwa kumbukumbu ya serikali na mkirejesha tutavihakiki kama vifaa vyote vipo ambavyo mmepewa na vilivyotumika. Kwahiyo, tuhakikishe vifaa vyote vinatunzwa” alisema Odero.

Zoezi la uandikishaji wa orodha ya wapiga kura litahusisha vifaa vifuatavyo, daftari la kuandikia wapiga kura, kalamu, penseli, kifutio, kibao cha wino, tisheti na kofia, mihuri na mabango ambavyo vinatarajiwa kutolewa tarehe 10 Novemba, 2024 katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.


MWISHO



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.