• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Maandalizi ya bajeti, RUWASA yatakiwa kukutana na Halmashauri za Dodoma

Imewekwa tarehe: March 10th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge ameutaka Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA Mkoa wa Dodoma katika bajeti yake kwa mwaka 2021/2022 kukutana na kila Halmashauri ili kujua mahitaji yao ili katika bajeti hiyo ilenge mahitaji mahususi kwa ajili ya kupunguza uhaba wa maji kwa wananchi.

Dkt Mahenge ametoa wito huo Machi 9, 2021 jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha wadau wa sekta ya maji na usafi wa mazingira vijijini Mkoa wa Dodoma iliyoandaliwa na RUWASA kwa lengo la kushirikiana na wadau katika kumaliza tatizo la maji.

Amesema kuna haja ya Wakala huo kurudi katika halmashauri ili kupata mahitaji halisi ya miradi ya maji kabla ya kupanga bajeti ya kutekeleza miradi mbalimbali katika Mkoa wa Dodoma.

“Mrudi kwenye Halmashauri kule chini wao ndio wanajua mahitaji halisi katika vijiji ili mnapopanga bajeti yenu ilenge katika maeneo yenye uhitaji, pia katika kila Wilaya hakikisheni kuna bwawa ambalo litaweza kuhudumia vijiji viwili vitatu” amesema Dkt Mahenge.

Aidha ameitaka RUWASA kuhakikisha inapita kijiji hadi kijiji ili kuona hali ya upatikanaji wa maji na mahitaji yake halisi ili kuingizwa katika mpango kazi wao katika bajeti ijayo ya Wakala huo.

Amesema kuna haja ya kuwa wabunifu sana na kuacha kufanyakazi kwa mazoea na katika malengo yao wahakikishe kila kijiji kinapata maji na kuongeza mtandao wa maji kwa wananchi ili huduma hiyo ipatikane kwa urahisi kwa wananchi.

”Lazima tuwe wabunifu kitengo cha ubunifu kiboreshwe kwani kwa sisi Mkoa wa Dodoma tuna maji sana chini ya ardhi na kipindi hiki cha mvua tunapoteza maji mengi sana tukiwa wabunifu haya maji yanayopotea yangesaidia sana” amesema.

Meneja wa Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA Mkoa wa Dodoma Dkt Godfrey Mbabaye amesema lengo la kikao hicho ni kukutana na wadau na watumiaji wa maji katika Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma ili kushirikishana katika mipango waliyoiweka kuona kama inatija katika maeneo wanayotoka wadau hao.

Ambapo RUWASA imewasilisha mipango yao kupitia maada zilizowasilishwa katika kikao hicho amesema RUWASA wana jumla ya miradi 167 ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na miradi 100 imekamilika sawa na asilimia 60.

Amesema hadi kufikia Desemba 2020 utoaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa vijijini ni asilimia 61.9 katika Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma, amebainisha kuwa hadi kufikia mwezi juni 2021 hali ya upatikanaji wa maji itaongezeka hadi kufikia asilimia 67.2.

Ameongeza ” RUWASA Mkoa wa Dodoma kwa mwaka 2020/2021 imetengewa kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 9.3 na mpaka mwezi Desemba 2020 Mkoa ulipokea zaidi ya shilingi bilioni 4.1 sawa na asilimia 44.6 na kati ya miradi hiyo 25 ni mipya, 80 ni ya ukamilishaji na ukarabati na kukamilika kwake itaongeza upatikanaji wa maji kwa asilimia 5.3.

Amebainisha kuwa katika bajeti ya 2021/2022 bajeti imelenga katika kutekeleza maagizo na maelekezo ya viongozi wa ngazi za kitaifa iliyotolewa katika maeneo husika, maeneo yasiyokuwa na huduma ya maji, miradi inayoendelea kujengwa, ukarabati wa miradi iliyopita mda wake au kuharibika na kupeleka maji katika huduma za kijamii.

Wakichangia maada katika kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma Jabir Shekimweri amesema kuna haja ya kukaa chini na kutafakari kwani kuna miradi mingi imetengewa fedha nyingi lakini miradi hiyo haikamiliki na wananchi wanaendelea kulia kwa kukosa huduma ya maji.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.