• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Majaliwa ataka nguvu zaidi uwezeshaji wananchi

Imewekwa tarehe: September 19th, 2022

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wadau wote wa uwezeshaji wananchi kiuchumi waongeze nguvu katika kutoa huduma za uwezeshaji hasa maeneo ya pembezoni ya miji na vijijini ili kufikia malengo ya nchi katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini.

Ametoa wito huo leo (Jumatatu, Septemba 19, 2022) wakati akifungua kongamano la sita la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, lililofanyika katika ukumbi wa PSSSF, Jijini Dodoma.

“Pamoja na wito huo, Mikoa ambayo imeanzisha vituo vya uwezeshaji iendelee kuboresha miundombinu ili vituo hivyo vikidhi ubora na viwango katika kutoa huduma za uwezeshaji”

Waziri Mkuu amesema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan madarani Serikali imeendeleza azma yake ya kuwawezesha wananchi ikiwemo utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu.

“Katika mwaka 2021/22, Serikali kupitia mifuko na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi iliwezesha utoaji wa mikopo ya masharti nafuu yenye thamani ya shilingi bilioni 903 kwa wanufaika wapatao milioni 5.9 nchi nzima”.

Vilevile, ameongeza kuwa katika mwaka 2021/2022 jumla ya watanzania 72,395 walipata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja kutokana na ushiriki wao kwenye miradi ya kimkakati na uwekezaji (Local Content). “Aidha, miradi ya kimkakati ilitoa kandarasi ndogo kwa kuingia mikataba na kampuni 2,019 za Watanzania kwa huduma mbalimbali.”

Pia, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka taasisi za fedha, mifuko na program za uwezeshaji zihakikishe zinapunguza riba za mikopo hadi kufikia kiwango cha tarakimu moja ili kukuza biashara na kuchochea uchumi.

Naye, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka na kuimarisha miundombinu ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ili kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.