• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Marufuku kulima mahindi, mtama katikati ya Jiji

Imewekwa tarehe: October 26th, 2018

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi amepiga marufuku kupanda mazao ya mahindi, mtama na uwele katika kata 20 ambazo zipo katikati ya Jiji la Dodoma.

Ametoa kauli hiyo jana alipokuwa akitoa taarifa ya Katibu wa Baraza katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa  Mwalimu Nyerere uliopo Chuo cha Maendeleo Vijijini kata ya Mnadani jijini hapa.

Kunambi alisema kuwa kata 20 ambazo zipo katikati ya Jiji la Dodoma haziruhusiwi kuendesha kilimo cha mazao marefu na badala yake mazao ambayo yanatakiwa kulimwa ni mazao ya bustani na mboga mboga.

“Kutokana na hadhi ya Jiji ni marufuku kuendesha kilimo cha mahindi, mtama na uwele katika kata 20 zilizopo katikati ya jiji ila kinaweza kufanyika kilimo cha bustani na mbogamboga. Jambo la muhimu ni kuhakikisha usafi ndani ya Jiji unazingatiwa” alisema Kunambi.

Akijadili taarifa ya katibu wa baraza la madiwani, diwani wa kata ya Majengo Mhe. Msinta Mayaoyao (CCM) ameshauri Jiji kufanya matangazo ya kuzuia wananchi wasifanye kilimo hicho na sio kusubiri wapande mazao na baadaye kuyafyeka.

“Suala la kutopanda mazao marefu ni la kisheria, lakini wapo watu ambao hawajui kama ni kosa kwa maana hiyo nashauri yafanyike matangazo kwa kila kata kama inavyofanyika kwenye siku ya usafi, itakuwa shida kubwa na kuna uwezekano wa kutengeneza migogoro na wananchi pale ambapo tutasubili watu waanze kupanda mazao yao na baadaye Jiji kuyafyeka.

“Wananchi wanatakiwa kupewa elimu mapema na kila diwani afanye wajibu wake wa kutoa elimu kwa wananchi ili wasiendelee kujishughulisha na kilimo cha mazao hayo na pia watendaji wa kata na mitaa wafanye kazi zao ikiwepo ya kuzuia wananchi kulima mazao hayo na wawahamasishe kulima mazao ya mbogamboga, nyanya na kadharika,” alisema Mhe. Msinta.

Aidha, Diwani wa kata ya Kiwanja cha ndege, Mhe. Amos Mbalanga (CCM) amemshauri Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji kuwachukulia hatua kali maofisa watendaji ambao wananchi ndani ya kata zao wanaendelea na kilimo ambacho hakitakiwi kisheria.

Akichangia taarifa ya mkurugenzi juu ya elimu, Diwani wa kata ya Kikombo Mhe. Yona Kusaja (CHADEMA) amesema kuwa ni wakati wa kuboresha elimu kwa kuzingatia zaidi upelekaji walimu wa kutosha katika shule hususani shule zilizopo vijijini.

Alisema ili kuboresha elimu ni vyema kuboresha miundombinu iwe rafiki kwa walimu ikiwa ni pamoja na kuboresha makazi yao, kuwapandisha madaraja, kuwapatia stahiki mbalimbali ambazo wanazihitaji na kupeleka walimu wa kutosha katika shule hizo.

Naye Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma,  Prof. Davis Mwamfupe akizungumza na baraza la madiwani alisema kuwa ili kuweza kuwa na baraza imara ni lazima kuwa na baraza lenye umoja na mshikamano katika masuala mazima ya kimaendeleo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.