• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mavunde ataka matokeo utafiti wa kilimo kuwafikia wakulima kwa wakati

Imewekwa tarehe: July 7th, 2022

NAIBU WAZIRI wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde ameielekeza Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kuhakikisha matokeo ya tafiti inazofanya yanawafikia wakulima kwa wakati ili kuongeza tija na kipato chao.

Naibu Waziri Mavunde ameyasema hayo leo tarehe 07 Julai, 2022 aliposhiriki Maadhimisho ya Siku ya Kilimo Biashara, Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika katika viwanja vya Selian vilivyopo Mkoani Arusha.

"TARI mnafanya kazi nzuri, lakini bado mnayo kazi kubwa ya kufikisha utaalamu na teknolojia mnazozigundua kwa wakulima wetu. Wekeni mkazo mkubwa katika kutangaza matokeo na teknolojia hizo ili ziweze kuwa na tija kubwa kwa wakulima.

Watafiti lazima waache utaratibu wa kufungia au kukaa  na matokeo ya tafiti na teknolojia maofisini, badala yake kujikita katika ubunifu zaidi wa kufikisha utaalamu huo kwa wakulima.

Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetupa kipaumbele cha kipekee sisi wakulima, na ndo maana bajeti ya Wizara ya Kilimo imeongezeka kutoka bilioni 294 mwaka 2021/2022 hadi bilioni 954 mwaka 2022/2023.

Bajeti hii iliyoongezeka imeelekezwa katika utekelezaji wa vipaumbele vya kimkakati ikiwemo kuimarisha utafiti, kuongeza uzalishaji wa mbegu bora ili kuongeza mavuno kwa wakulima sambamba na ugunduzi wa mbinu bora za kilimo ili kumsaidia mkulima wa Tanzania kuzalisha kwa tija”. Alisema Mavunde.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TARI, Dkt. Geoffrey Mkamilo alieleza kuwa wamepokea maelekezo hayo ya Mhe. Mavunde na kwamba wameanza utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na kuanzisha maadhimisho ya siku ya kilimo biashara katika vituo vyote vya Kanda vya Utafiti na Viwanja vya Nanenane Nchi nzima, lengo likiwa ni kufikisha matokeo ya tafiti mbalimbali kwa wakulima kwa wakati ili kukidhi malengo tarajiwa ya kumsaidia mkulima wa Tanzania kulima kwa tija.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.