• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mbunge Mavunde agawa Kompyuta na Printa Shule za Sekondari za Serikali Dodoma

Imewekwa tarehe: March 18th, 2025

Na. Leah Mabalwe, VIWANDANI

Wanafunzi wa shule za sekondari za serikali waaswa kuongeza jitihada katika masomo yao ili kuzidisha ufaulu.

Hayo yalisemwa na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde wakati wa hafla ya ugawaji wa komputa na printa katika shule zote za serikali za sekondari jijini Dodoma na uzinduzi wa maabara ya kisasa ya kompyuta ya Shule ya Sekondari Viwandani. 

“Napenda kuhamasisha wanafunzi wote wa shule za sekondari kuongeza jitihada sana katika masomo yenu. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sasa anawekeza sana katika sekta ya elimu ili wanafunzi wote mpate mazingira mazuri kwa ajili ya kujisomea. Kwa sasa tunahitaji kujenga Jiji la Dodoma katika sekta ya elimu na kazi kubwa bado zinaendelea kufanyika. Nimeamua kufanya ziara hii ya ugawaji wa kompyuta katika shule zote za Dodoma mjini ili kuwaongezea maarifa pamoja na kukua kwa utandawazi kwasababu tunarahisisha upataji wa maarifa kwa ninyi wanafunzi wote. Kompyuta hizi zina kila kitu ambacho wanafunzi mnahitaji kujifunza. Hivyo, niwasisitize sana kuongeza juhudi katika masomo yenu” alisema Mavunde.

Akiongelea suala la watoto wenye ulemavu alisema kuwa nao wanafursa ya kupata elimu kama watoto wengine. “Na sitoishia hapa nina mpango pia wa kuwasaidia watoto wenye mazingira magumu pamoja na watoto wenye ulemavu wa Jiji la Dodoma kwa kugawa madaftari bure pamoja na mabegi ya mgongoni, suala hilo lipo katika mchakato hivyo basi, serikali yetu kwa sasa imejipanga kikamilifu kukemea ubaguzi wa watoto wenye ulemavu” alisema Mavunde. 

Nae, Mkuu wa Shule ya Sekondari Viwandani, Ester Simchimba alimshukuru Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mchango wao mkubwa wa kuboresha miundombinu ya shule hiyo.

“Tunakushukuru mbunge wetu kwa kufika katika shule yetu kwaajili ya hafla ya utoaji wa vifaa vya Kompyuta pamoja na printa lakini pia kwa ajili ya uzinduzi wa maabara ya kisasa. Kwa niaba ya uongozi wa shule pamoja na kamati ya wazazi tunakushukuru sana kwa kuwa mdau mkubwa wa maendeleo ya shule yetu kwasababu umeshirikiana na serikali katika kuboresha miundombinu ya shule na hata kupelekea kuongezeka kwa ufaulu mzuri kwa wananafunzi, tunakushukuru sana mbunge wetu” alisema Mwl. Simchimba.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.