• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkandarasi wa REA akatwe malipo - Waziri Kalemani

Imewekwa tarehe: August 12th, 2020

WAZIRI wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, ameagiza mkandarasi anayetekeleza mradi wa umeme vijijini, Awamu ya Tatu, mzunguko wa kwanza, mkoani Dodoma akatwe asilimia 10 ya malipo yake kutokana na kuchelewa kukamilisha kazi hiyo.

Waziri Kalemani ametoa agizo hilo leo, Agosti 12, 2020 baada ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Chemba.

Akiwa amefuatana na Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga, Waziri Kalemani ameutaka uongozi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kukata kiasi hicho cha malipo ya mkandarasi Kampuni ya A2Z Infra Engineering Limited, kuanzia Juni 30, 2020 muda ambao alipaswa kukamilisha mradi.

Sambamba na hilo, Waziri  pia amemtaka mkandarasi  huyo kukamilisha kazi ya kuunganisha umeme katika vijiji vyote 66 vilivyobakia kabla ya Septemba 15 mwaka huu, huku akisisitiza kuwa, hakutakuwa na nyongeza ya muda wala msamaha.

"Asipomaliza ndani ya wakati huo, mchukulieni hatua za kisheria na kimkataba. Maeneo yatakayobaki fanyeni ninyi TANESCO kwa pesa hiyo".

Aidha, amemwagiza mkandarasi huyo kuongeza vibarua na magenge, ili aweze kukamilisha kazi kwa wakati.

Vilevile, amemtaka kuondoa mara moja nguzo zote zilizorundikana chni na kuzisimika, kuvuta  nyaya na kuwaunganishia umeme wananchi.

"Kiu ya wananchi ni kuona umeme unawaka katika nyumba zao. Hawapendezewi kuona nguzo zikiwa zimerundikana chini, nanyi mkipitapita pasipo kuwawashia umeme", amesisitiza Waziri.

Dkt. Kalemani ametoa wigo kwa wakandarasi wote nchini, wonaondelea na kutekeleza Miradi ya REA III, kuhakikisha wanakamilisha ifikapo Septemba 15, 2020

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya amemshukuru Waziri kwa kufuatilia utekelezaji wa mradi wa REA huku akiweka wazi kuwa hana imani na mkandarasi huyo kutokana na kutotekeleza majukumu yake ipasavyo.

Mkuu huyo wa Wilaya ameahidi kufanyia kazi maelekezo ya Waziri katika kumsimamia mkandarasi huyo anayefanya kazi katika Wilaya yake.

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani akitoa maagizo mbele ya mkandarasi na timu ya Wilaya ya Chemba kuhusu utekelezaji wa mradi wa REA.


Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani (wa pili kulia) akimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Chemba Simon Odunga (wa pili kushoto) akifafanua jambo wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati kutembelea utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Wilayani Chemba mkoani Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.