• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkoa waridhishwa kasi ya upandaji miti jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: January 24th, 2021

UONGOZI wa Mkoa wa Dodoma umeridhishwa na muendelezo wa utekelezaji wa kampeni ya kijanisha Dodoma unaofanywa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo kwa lengo la kulinda na kutunza mazingira.

Kauli hiyo ilitolewa na mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Natalius Linuma alipokuwa akitoa shukrani kwa washiriki wa zoezi la upandaji miti kwa timu “B” lililofanyika katika shule ya msingi Ipala jijini hapa.

Linuma ambaye pia ni Katibu Tawala msaidizi, anayesimamia menejimenti ya Serikali za Mitaa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, alisema kuwa mheshimiwa mkuu wa mkoa aliagiza kila mtumishi apande miti angalau 10 kila siku ya Jumamosi. Aidha, aliipongeza halmashauri ya jiji hilo kwa muitikio huu ambao ni utekelezaji wa agizo la mheshimiwa Mkuu wa Mkoa. “Sasa wito wangu kwenu ni kuitunza miti hii na kuhakikisha inakuwa. Ili kampeni hii itoe mafanikio makubwa haraka lazima tuongeze kasi ya upandaji miti na kuitunza” alisema Linuma.

Mwakilishi huyo, aliupongeza uongozi wa kata ya Ipala kwa kuwa mstari wa mbele katika upandaji miti. “Hapa Kata ya Ipala mmejitahidi sana kupanda miti, naona idadi ya miti iliyopandwa ni kubwa na inaendelea vizuri. Natamani Kata zote ziige mfano wa kata hii” alisema Linuma.

Awali mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Joseph Mabeyo (pichani juu) alisema kuwa jumla ya miti 1,500 ilipandwa katika zoezi la upandaji miti katika Kata ya Ipala.

Mwalimu Mabeyo ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa katika zoezi hilo, limehusisha upandaji wa miti ya matunda. “Wote tumeshuhudia katika zoezi hili tumepanda pamoja na miti mingine, miti ya matunda. Lengo ni kuboresha lishe ya wanafunzi. Wanafunzi wanapokuwa na afya njema inawawezesha kupata maarifa na ujuzi kwa uhakika. Hivyo, lishe bora itawafanya wanafunzi kuwa huru dhidi ya magonjwa na kutumia muda wao vizuri katika masomo” alisema Mwalimu Mabeyo.

Matunda pia ni sehemu ya chakula, hivyo yatakapokuwa na kukomaa yatawavutia wanafunzi kuyatumia kama matunda na chakula. Matumaini ya halmashauri ni kwamba, matunda haya yatasaidia kuondoa utoro kwa wanafunzi, aliongeza.

Nae mratibu wa kampeni ya kijanisha Dodoma, katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa halmashauri ilizigawanya timu mbili za watumishi wa halmashauri ili kuharakisha zoezi la upandaji miti. Alisema kuwa timu “A” iliongozwa na Mkurugenzi wa Jiji na timu “B” iliongozwa na Mkuu wa Idara ya Elimu Msingi.

Zoezi la upandaji miti katika shule ya msingi Ipala iliyopo Kata ya Ipala lilishirikisha watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi wa Jiji, Mthibiti ubora wa wilaya, Tume ya Utumishi wa Walimu, Wakala wa Misitu Tanzania, Kata ya Ipala na wananchi kwa ujumla.

Mthibiti Ubora wa Elimu Wilaya ya Dodoma Mjini, Mwalimu Lucy Mbolu akisiriki kupanda mti wake wa 11 wa mpapai katika shule ya msingi Ipala iliyopo jijini Dodoma katika utekelezaji wa kampeni ya Kijanisha Dodoma

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.