• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

Imewekwa tarehe: May 23rd, 2025

Na. Aisha Ibrahim, MADUKANI

MIKOPO ya asilimia 10 isiyo na riba kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa na tija kwa vikundi vya wajasiriamali na kuwasaidia kukuza kipato na kuinua uchumi katika Kata ya Madukani.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii, Kata ya Madukani, Asha Hussein alipokuwa akiongelea mikopo hiyo na umuhimu wake kwa wananchi wa kata ya madukani. 

Alisema kuwa katika kata hiyo kuna jumla ya vikundi 14 vilivyopatiwa mkopo wa kiasi cha shilingi milioni 273, ambapo wanawake ni vikundi saba na walipata kiasi cha shilingi milioni 160 na vijana ni vikundi saba waliopokea kiasi cha shilingi milioni 113.

Alisema kuwa kutokana na mikopo hiyo wanufaika wameweza kuanzisha shughuli mbalimbali zinazowaingizia kipato na kuweza kujiinua kiuchumi. “Asilimia kubwa wana vikundi na wameanzisha shughuli zao za kuwaingizia kipato. Mfano; kuna baadhi yao wanauza nguo, kuna vijana wamefungua duka la madawa, ufundi wa simu na baadhi ya wakina mama wanajishughulisha na ushonaji na wamefungua saluni za kike, mbali zaidi wapo wengine wanafanya shughuli za ufugaji nje ya kata hii” alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikundi cha Vijana cha Edame, William Frank, kutoka Kata ya Madukani, alisema kikundi hicho kinajishughulisha na ufundi wa kompyuta, funguo na simu, na kupitia mkopo wa asilimia 10 wameweza kununua vifaa kwaajili ya kuendeshea shughuli zao na kufanikiwa kuajiri baadhi ya vijana wenye ujuzi katika fani hiyo. “Kupitia mkopo wa asilimia 10 kwa vijana, tumeweza kununua vifaa vya kuendeshea shughuli zetu, mbali zaidi tumeajiri mpaka vijana wenye taaluma ya ufundi na wanafanya kazi vizuri” alisema Frank.

Vilevile, aliwaasa vijana kuwa na hali ya uthubutu hata kama hawana mitaji ya kujiajiri waweze kujitoa kufuata taratibu za kupata mikopo hiyo itakayowasaidia kuendesha maisha yao kwasababu haina riba. “Niwaase vijana wenzangu hata kama hawana mtaji wa kuanzisha shughuli yoyote twende tukaombe mikopo hiyo isiyo na riba, hii itasaidia tuweze kujiajiri wenyewe na kuweza kuendesha maisha yetu ya kila siku” alisema Frank. 

Nae, mnufaika wa mikopo hiyo, Elizabeth Sebastian, kutoka Kikundi cha Wanawake cha Amani, alifafanua kuwa kikundi hicho chenye jumla ya wanachama watano, walifanikiwa kupata mkopo wa kiasi cha shilingi 10,000,000 uliowasaidia kufanya maendeleo na kujikwamua kiuchumi. “Mkopo huu tulioupata tulifanikiwa kuanzisha mradi wa asali na tulikuwa na mizinga ya nyuki, lakini kutokana na changamoto tukaamua kufungua duka la nguo na kupitia mkopo tulioupata mara ya pili duka letu limekuwa kubwa na tumeweza kujikwamua kiuchumi. Kupitia mikopo hii tunaweza kutunza familia zetu na kutimiza majukumu mbalimbali ya hapa na pale. Pia tunapambana kuepuka kuwa tegemezi katika jamii kwasababu maendeleo katika jamii yanakuja kutokana na juhudi za kupambana” alisema Sebastian.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.