• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkuu wa Wilaya Apongeza Ujenzi wa Madarasa Mtumba

Imewekwa tarehe: September 22nd, 2024

Na. Valeria Adam, Dodoma

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, ametembelea miradi ya serikali iliyopo Kata ya Mtumba na kusisitiza elimu kuwa agenda ya kudumu.

Akizungumza na walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mtumba alitoa wito kwa jamii kufuatilia kwa karibu maendeleo ya kitaaluma, ufundishaji na ujifunzaji ili kuhakikisha majengo mazuri yaliyojengwa yanaakisi ubora wa elimu.

Alisema kuwa ni muhimu katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata elimu bora na yenye tija, na kwamba walimu wana nafasi kubwa katika kufanikisha hilo. “Nisisitize agenda hii ya elimu iwe ni ya kudumu, fuatilieni kwa karibu maendeleo ya kitaaluma, ufundishaji ili kusudi majengo haya mazuri tuliyojengewa yaakisi katika ubora wa elimu” alisema Alhaj Shekimweri.

Aidha, aliwapongeza walimu kwa kazi nzuri wanayoifanya na kuwataka waendelee kuwafundisha watoto kwa upendo na kwa kuwajali ili kuwasaidia watoto kujifunza vizuri bila kuhofia chochote. “Walimu muwafundishe watoto kwa upendo, muwaelekeze kwa kuwajali, muwasimamie katika maendeleo yao ya kitaaluma. Pia muwashirikishe wazazi ili waweze kujua tabia na mienendo ya watoto wao katika taaluma” alisisitiza Alhaj Shekimweri.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mtumba, Mwl. Kepha Kitutu alisema kuwa mradi wa ujenzi wa vyumba saba vya madarasa umesaidia katika kutatua changamoto ya upungufu wa madarasa. Alisema kuwa mradi umekamilika kwa asilimia 100 bila kuwa na deni lolote kutoka kwa wazabuni au mafundi ujenzi wa shule hiyo.

“Shule hii ina jumla ya wanafunzi 1,438 (wavulana 699 na wasichana 739), kabla ya mradi ilikuwa na vyumba 31 vya madarasa pekee. Hali ya madarasa ilikuwa mbaya sana, na baadhi yalikuwa chakavu na kuhatarisha usalama wa wanafunzi na walimu. Hivyo, kusababisha mrundikano mkubwa wa wanafunzi.

“Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na madawati 30 kutoka mradi wa EP4R umekamilika kwa asilimia 100. Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa kutoka mapato ya ndani umekamilika kwa asilimia 100. Ujenzi na utekelezaji wa mradi huu umekamilika kwa asilimia 100 bila ya kubaki na deni lolote kutoka kwa wazabuni au mafundi ujenzi” alihitimisha Mwl. Kitutu.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.