• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Moto wateketeza nyumba Dodoma, DC anena

Imewekwa tarehe: July 18th, 2021

MKUU wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Jabir Shekimweri amewataka Wananchi wa Kata ya Viwandani kuchukua kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto ikiwa ni pamoja na kumiliki na kujua kutumia vizimia moto (Fire Extinguishers).

Mhe. Shekimweri ameyasema hayo alipotembelea eneo kulipotokea moto usiku wa kuamkia leo (tarehe 18 Julai, 2021) ba kuteketeza nyumba moja nayomilikiwa na Abduelly Mstahafu na sehemu ya kulala wageni ya ‘Holiday Guest House’. Mkuu wa Wilaya aliongozana na Diwani wa Kata ya Viwandani Mhe. Jaffary Mwanyemba na Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wa Mkoa wa Dodoma Deogratias Inano.

Aidha, Mheshimiwa Shekimweri aliwataka wananchi kujitahidi kukatia bima ya moto nyumba zao ili inapotokea hasara kama hiyo Bima waweze kuwalipa. Akihitimisha nasaha zake, Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya aliwaasa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya UVIKO-19 vinavyosababisha ugonjwa wa Korona kwa kuvaa barakoa wanapokuwa katika mikusanyiko, kuzingatia umbali kati ya mtu na mtu na kunawa kwa sabuni na maji safi tiririka.”

Uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (M) Dodoma kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi umebaini chanzo cha moto ulioteketeza nyumba hiyo iliyopo mtaa wa Baruti kata ya Viwandani jijini Dodoma kuwa ni Sigara

Akizungumza baada ya Uchunguzi Mkaguzi Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (M) Dodoma Deogratias Inano amesema, chanzo cha moto huo ni sigara iliyokuwa ikivutwa na mtoto wa mwenye nyumba aliyejulikana kwa jina la Mohamed Omari (35) ambaye ana matatizo ya akili.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye ni dada yake na Mohamed amesema, alimuona kaka yake akitokea chumbani na baada ya muda mfupi chumba kilianza kuwaka moto.

Alisema kuwa kaka yake huyo huwa ana tabia ya kuvutia sigara ndani na mara ya mwisho alimuona akiingia ndani na sigara kama ilivyo kawaida yake na alipotoka ndani ndipo alipoona dalili ya moto katika chumba kile

“Nilimuona kaka Muddy akivuta sigara na kuingia nayo ndani, baada ya muda mfupi alitoka na ndipo tulipoona dalili ya moto katika chumba kile. Nilipoenda kuangalia nilikuta godoro limeshika moto na ndipo moto ulipotuzidi na kuteketeza nyumba” Alisema dada huyo.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Jabir Shekimweri (katikati) akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Viwandani kulipotokea moto na kuteketeza nyumba. Kulia ni Mheshimiwa Jaffary Mwanyemba, Diwani wa Kata ya Viwandani ilipo nyumba hiyo, na Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma Deogratias Inano (kushoto).

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.