• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mradi wa Majisafi Ntyuka Chimalaa wazinduliwa

Imewekwa tarehe: June 1st, 2023

BODI mpya ya Wakurugenzi ya tisa ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), imeagizwa kupunguza upotevu wa maji kutoka asilimia 28 hadi kufikia chini ya asilimia 20 wakati ikizinduliwa leo Alhamisi Juni 1, 2023.

Agizo hilo, limetolewa na Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi mara baada ya kuzindua bodi hiyo na mradi wa Majisafi Ntyuka Chimalaa wenye thamani ya Shilingi Bilioni 471.8.

Mhandisi Nahundi ameiagiza bodi mpya ya tisa kushirikiana na watumishi kuweka mikakati ya kuendelea kuongeza makusanyo ili mamlaka iweze kuboresha utoaji wa huduma huku akiipongeza bodi ya nane iliyomaliza muda wake kwa kuongeza makusanyo kutoka Shilingi Bilioni 1.7 hadi Shilingi Bilioni 2.2 kwa mwezi.

Naibu waziri huyo amewata kuendelea kuwahudumia ipasavyo wakazi wa Dodoma huku ikitekeleza miradi ya muda mfupi ya kupunguza changamoto ya ukosefu wa maji wakati Serikali ikitekeleza miradi mikubwa.

Pia, ameiambia bodi hiyo kushirikiana na Menejimenti ya DUWASA kuendelea kusimamia ipasavyo miradi yote ya maji pamoja na kuhakikisha uwepo wa thamani ya fedha katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali, akizungumza mara baada ya kuzindua mradi wa maji, Naibu Waziri Mahundi ameeleza dhamira ya Rais kumtua mama ndoo kichwani inaendeea kutekelezwa kwa vitendo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameshauri Dodoma kupewa mpango mkakati wa kipekee wa kutatua changamoto ya maji ili kuendana na uwepo wa makao makuu ya nchi.

Amesema Mkoa wa Dodoma kuna taasisi nyingi ambazo wanafanya nazo kazi huku akiitaja DUWASA kama Mamlaka inayofanya kazi kwa ufanisi mkubwa.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi, Mkurugenzi Mtendaji wa DUWASA, Mhandisi Aron Joseph amesema mradi huo unanufaisha wakazi wapatao 4,441 ambapo kati ya hao 1,931 wanaishi katika maeneo ya Ntyuka mtaa wa Chimalaa katika awamu ya kwanza, na awamu ya pili itanufaisha wakazi wapatao 2,510 katika mtaa wa Nyerere.

Mwenyekiti wa Bodi aliyemaliza muda wake, Profesa Faustine Bee amesema katika kipindi cha uongozi wao wamepata mafanikio mbalimbali ikiwemo kuongeza urefu wa mtandao wa mabomba ya kukusanya majitaka. Naye, Mwenyekiti mpya wa bodi, Balozi Job Masima amemshukuru Waziri wa Maji, Jumaa Aweso kwa kutekeleza kwa vitendo adhma ya kuhakikisha wananchi wanafikiwa na huduma ya maji karibu zaidi katika maeneo yao.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.