• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Msiuze ardhi kiholela, shirikisheni Jiji - DC Maganga

Imewekwa tarehe: August 16th, 2020

WANANCHI wilayani Dodoma mjini wameshauriwa kutouza ardhi kiholela badala yake kupata msaada wa kisheria kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini, Mwalimu Josephat Maganga alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Kata ya Mtumba jijini Dodoma jana katika ziara yake ya kujitambulisha, kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Mwalimu Maganga alisema “ndugu zangu wapendwa wana Mtumba pamoja na mitaa yetu yote minne, Vikonje ‘A’, Vikonje ‘B’, Majengo na Mtumba, hii ardhi tunayoiona kama wanavyosema, zamani haikuwa na thamani. Lakini tumekuja kugundua kwamba ina thamani kubwa. Wananchi tunaongezeka, tunakuwa wengi lakini ardhi ipo hivyo hivyo. Hii ardhi ni kitu cha thamani, ina thamani kiuchumi, tunalima kwenye ardhi hii tunapata chakula, tunajenga kwenye ardhi hii nyumba zetu na tunaishi, tumezaliwa kwenye ardhi hii na inawezekana, na ni kweli kabisa kwamba hata kufa tutazikwa kwenye ardhi hii”.

Alisema kuwa ardhi ni kitu cha thamani na yanapofanyika maamuzi ya ardhi wanaoyafanya wahakikishe wanafanya maamuzi sahihi. Aidha, aliwataka Wenyeviti wa Mitaa na watendaji kuwa makini na uuzaji ardhi. “Ndugu zangu naomba tuwe makini na uuzaji holela wa ardhi, tuwe makini sana. Hata kama mwananchi wa kawaida anataka kuuza eneo lake, sheria zinaturuhusu kuhoji, kwa sababu anaweza akauza ardhi hapa, mkashitukia anakuja mtu anatengeneza mambo ya baruti hapa, ukimuuliza anasema anapasua miamba hapa halafu anasababisha matatizo. Tutahitaji kujua huyo mtu ni nani? anatoka wapi na kwanini aje anunue ardhi kubwa hapa. Kuna wakati mwingine wanakuja watu wataalam kuwazidi hata nyie wenyewe. Niwaombe kabla ya kufanya maamuzi shirikisheni Halmashauri ya Jiji, lazima itatoa msaada wa kisheria” alisema Mwalimu Maganga.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutenga shilingi milioni 210 kwa ajili ya kulipa fidia wananchi waliotwaliwa maneo yao. “Nafurahi kuona hawa wananchi 34 wanapata fidia zao shilingi milioni 210. Niipongeze Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutenga fedha hizo ambazo nimetaarifiwa zitalipwa mwezi huu” alisema Mwalimu Maganga.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini, Mwalimu Josephat Maganga akisisitiza jambo alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Kata ya Mtumba jijini Dodoma jana (16/08/2020) katika ziara yake ya kujitambulisha, kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.