• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino kinara usafi wa Mazingira- Dodoma

Imewekwa tarehe: May 27th, 2023

Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO

MTAA wa Mwaja uliyopo Kata ya Chamwino umepongezwa kwa juhudi zake za usafi wa mazingira na kupewa cheti na Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuthamini juhudi hizo.

Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa kata ya Chamwino, Jumanne Ngede alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kushiriki usafi wa mazingira katika Mtaa wa Mwaja uliopo Kata ya Chamwino jijini Dodoma.

Ngede alisema kuwa amefurahishwa na muitikio mkubwa wa wananchi katika zoezi la usafi wa siku ya Jumamosi. “Mtaa wa Mwaja umeingia katika rekodi ya mtaa msafi katika mazingira kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Hongera sana, lakini msirudi nyuma katika suala la usafi. Tuendelee kuhimizana kufanya usafi wa mazingira. Wananchi wote tunafahamu kuwa kufanya usafi ni kwamujibu wa sheria, lakini kwa wakazi wa Mwaja usafi ni jadi yetu” alisema Ngede.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Usafi na usimamizi wa taka katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alimtaja Diwani huyo kuwa wa mfano katika kusimamia usafi wa mazingira. “Niwapongeze sana mnavyodumisha usafi kila Jumamosi ili kuhakikisha mazingira ya mitaa na kata yanakuwa safi. Mazingira safi yanatuepusha na magonjwa ya mlipuko hasa kipindupindu. Mtakumbuka tangu tumeanza kutekeleza kampeni ya usafi, ugonjwa wa kipindupindu umekuwa historia katika Jiji la Dodoma” alisema Kimaro.

Akiongelea maeneo yaliyosanyiwa usafi katika zoezi hilo, alisema kuwa usafi umefanyika katika maeneo mbalimbali ya Mtaa wa Mwaja. “Miongoni mwa maeneo yaliyofanywa usafi wa pamoja ni eneo la makaburi ya Hijra. Niwapongeze kwa mara nyingine wote mlioshiriki zoezi la usafi katika makaburi haya. Imani yangu kufanya usafi katika eneo walipolala wenzetu waliotangulia ni sehemu ya ibada kwa sisi tulio hai” alisema Kimaro.

Ikumbukwe kuwa tarehe 11 Mei, 2023 Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lilitoa pongezi na vyeti kwa mitaa minne iliyofanya vizuri katika ushiriki wa viongozi na wananchi katika usafi wa mazingira Mtaa wa Mwaja kutoka Kata ya Chamwino ukiwa miongoni kwa kipindi cha robo ya tatu (Januari-Machi), 2023.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.