• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mwenyekiti UWT Taifa awataka wanawake kuchangamkia mikopo ya Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: November 2nd, 2024

Na. Faraja Mbise. DODOMA

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda amewataka wanawake wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuachana na mikopo ya Kausha damu na mwendokasi inayowanyanyasa na kuwadhalilisha wanawake kutokana na muda wa marejesho na kiwango cha riba kuwa kikubwa na hivyo kushindwa kujikwamua kiuchumi na kuwaongezea umasikini zaidi.

Kauli hiyo aliitoa wakati akizungumza katika Uzinduzi wa Umoja wa Wanawake Wafanyabiashara Masoko yote katika Jiji la Dodoma (UWAWAMA), uliofanyika Cathedral Social Hall, tarehe 01 Novemba, 2024.

Chatanda aliwataka wanawake wafanyabiashara kuachana na mikopo ya kausha damu na kujiunga na vikundi ili kupata mikopo ambayo inatolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma. "Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluh Hassan imerejesha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa utaratibu ulioboreshwa zaidi ikiwemo kutumia benki kwa halmashauri kumi za majaribio zikiwemo za Dodoma" alisema Chatanda.

Kuhusu mikopo ya kausha damu, aliwataka wafanyabiashara kuachana nayo kwasababu inarudisha uchumi wa nchi nyuma na mwanamke anashindwa kujikwamua kiuchumi kutokana na masharti magumu ya riba na muda uliowekwa katika mikopo hiyo. "Sasa nawahimiza kuchangamkia fursa ya mkopo usio na riba tuliyopewa na serikali na kuondokana na mikopo ya kausha damu, ujinga na mwendokasi inayowanyanyasa na kuwadhalilisha wanawake kutokana na utaratibu wa mikopo hiyo ukiwemo muda wa marejesho na kiwango kikubwa cha riba kuwa kikubwa hivyo badala ya kujikwamua kiuchumi inaongeza umaskini zaidi" alisisitiza Chatanda.

Katika kuhamasisha wanawake walengwa wa mikopo, alitoa rai kwa viongozi wanawake kuhamasisha wachangamkie fursa ya mikopo inayotolewa na serikali. "Natoa wito kwa viongozi wanawake kuhamasisha walengwa wa mikopo hii wachangamkie fursa ya mikopo inayotolewa na serikali yao" alisisitiza Chatanda.

Aidha, aliwashukuru wanawake wa nchi nzima kuitikia wito wa kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024.

"Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inaonesha wanawake walioandikishwa ni asilimia 51.29 na asilimia 48.71 ni wanaume. Asanteni sana wanawake kwa kuiheshimisha serikali, kiongozi wetu mkuu wa nchi pamoja na mimi mwenyekiti wenu ambaye wakati wa ziara zangu zote nimekuwa nikiwasihi wanawake na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha" alieleza Chatanda.

Uzinduzi wa umoja wa wanawake wafanyabiashara masoko yote katika Jiji la Dodoma ulihudhuriwa na wanawake wa masoko mbalimbali kama Soko kuu la Job Ndugai, Sabasaba, Majengo, Machinga na Bonanza. Pia na vikundi mbalimbali kama Wanawake na Samia, wanawake na Nyerere, Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Dodoma Jiji (JUWAKIDO).



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.