• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yawaasa wahariri wa vyombo vya habari kutumia kalamu kulinda amani ya taifa

Imewekwa tarehe: September 15th, 2025

Na. Noel Rukanuga, DODOMA

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imewataka wahariri wa vyombo vya habari nchini kutumia kalamu zao kwa uadilifu, kwa kuzingatia maadili ya taaluma na kuhakikisha wanahabarisha umma kwa namna inayolinda amani na usalama wa taifa.

Akizungumza wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili kati ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wahariri wa vyombo vya habari, kilichofanyika leo Septemba 12, 2025 katika Ukumbi wa Mkemia Mkuu wa Serikali, jijini Dodoma, Mkurugenzi Msaidizi wa Uratibu na Huduma za Ushauri wa Kisheria, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Ipyana Mlilo, amesema kuwa sekta ya habari ni mhimili muhimu katika maendeleo ya taifa, hivyo kikao kazi hicho kimetoa nafasi ya kuimarisha ushirikiano baina ya wahariri na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, ili kuendelea kutoa elimu ya kisheria kwa jamii kwa weledi. 

“Kikao hiki kimekuwa na manufaa makubwa katika kuhakikisha jamii inapata uelewa mpana kuhusu masuala ya kisheria. Tumejadiliana mambo mengi muhimu ambayo yatashughulikiwa kwa lengo la kuelimisha na kulinda maslahi ya umma,” alisema Mlilo.

Alisisitiza umuhimu wa waandishi wa habari kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia maadili ya taaluma na kuhakikisha wanachangia katika ustawi na usalama wa taifa.

Akiwasilisha taarifa ya majukumu ya Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA), Rais wa Chama hicho Bavoo Junus, amesema kuwa kuwa TPBA ni Chama muhimu katika kusimamia, kulinda na kutetea maslahi ya Serikali na rasilimali zake.

Alibainisha kuwa TPBA ni chama cha kitaaluma kinachowaunganisha wanasheria wote wanaohudumu katika taasisi za umma ikiwemo Wizara, Halmashauri, Wakala, na Mashirika ya umma pamoja na Kampuni ambazo Serikali inamiliki hisa.

“Kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, TPBA imefanikiwa kueneza elimu ya sheria kwa wananchi wote Tanzania Bara na Zanzibar,” alisema Junus.

Aliongeza kuwa TPBA limeanzisha jukwaa la mawakili wa serikali kwa ajili ya kubadilishana uzoefu kitaaluma, kujadili changamoto, na kuweka mikakati ya pamoja ya kutetea maslahi ya Serikali.

Pia alieleza kuwa chama hicho hutoa mafunzo endelevu kwa wanachama wake ili kuongeza uelewa na ufanisi wa kiutendaji, badala ya kutegemea waajiri pekee.

Junus alieleza kuwa TPBA ilianzishwa kwa mujibu wa Kifungu cha 16A (1) cha Sheria ya Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Sura ya 268, pamoja na Tangazo la Serikali Na. 589 la tarehe 16 Agosti 2019.

Aidha, alifafanua kuwa TPBA ni tofauti na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), ambapo TPBA uwakilisha wanasheria wa Serikali, wakati TLS hujumuisha wanasheria wote nchini, bila kujali mwajiri.

Alisema kuwa chama wa TPBA unategemea ajira ya mwanachama katika utumishi wa umma, wakati TLS huruhusu wanachama wake kuendelea hata baada ya kutoka kazini.

Akizungumza kwa niaba ya wahariri walioshiriki kikao kazi hicho, Mhariri Mkuu wa Clouds Media, Joyce Shebe, alipongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuratibu kikao hicho ambacho kimetoa maarifa na uelewa kuhusu masuala ya kisheria kwa wahariri, jambo litakalosaidia kuboresha utekelezaji wa majukumu yao.

“Tunathamini nafasi hii ya kushirikishwa katika kujadili masuala ya sheria ambayo ni msingi wa kazi zetu. Tunatarajia ushirikiano huu uendelee,” alisema Shebe.

 




Matangazo

  • REQUEST FOR EXPRESSION OF INTEREST (EoI) (SELECTION OF AN INDIVIDUAL CONSULTANT September 19, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR RECRUITMENT OF URBAN TRANSPORT PLANNING SPECIALIST FOR THE CITY COUNCIL OF DODOMA (CCD) September 19, 2025
  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • RC. Senyamule atoa wito kwa wadau wa ushirika kushiriki uchaguzi mkuu

    September 22, 2025
  • Wakurugenzi watakiwa kutenga maeneo yatakayowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika kilimo

    September 21, 2025
  • Wakurugenzi watakiwa kutenga maeneo yatakayowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika kilimo

    September 21, 2025
  • Halmashauri za Dodoma zatakiwa kubuni vyanzo vipya vya mapato

    September 20, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.