Na James Mwanamyoto - Tanga
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amekabidhi hundi yenye thamani ya Bilioni 2.761 kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vilivyonufaika na mkopo wa asilimia 10, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hasan aliyoitoa kwa wananchi kuwa ataitekeleza ndani ya siku 100 za uongozi wake.
Prof. Shemdoe amekabidhi hundi hiyo kwa vikundi hivyo jijini Tanga katika Uwanja wa Tangamano, mara baada ya kukagua shughuli za wajasiriamali walionufaika na mikopo ya asilimia 10 mkoani Tanga.
“Leo tumetoa Bilioni 2.761 kwa vikundi vya halmashauri ya jiji la Tanga, Korogwe Mji, Korogwe wilaya , Lushoto, na Pangani, ambazo zitanufaisha vikundi vya wanawake 155, vijana 71 na wenye ulemavu 19 ambapo jumla ya ajira 1,715 zimetengenezwa,” amefafanua Prof. Shemdoe
1 CDA Street, 40477
Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA
Simu: +255 26 232 4817
Simu ya kiganjani:
Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz
Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.