• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais aipa tuzo maalum benki ya NMB

Imewekwa tarehe: August 20th, 2023

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan ametoa tuzo maalum kwa Benki ya NMB katika kutambua mchango na utendaji mzuri wa taasisi hiyo ya fedha nchini.

Akizungumza katika kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma kinachofanyika katika ukumbi wa mikutano wa AICC jijini Arusha, Rais Samia amesema pamoja na kuwapongeza wale waliofanya vizuri, serikali pia itafanya tathmini ya utendaji wa taasisi na mashirika mengine nchini.

“Kupitia mashirika, serikali inaweza kukusanya fedha nyingi za kutosha kujazia upungufu wa bajeti ya nchi na hivyo kuipunguzia serikali mzigo wa kwenda kukopa nje,” alisema Dkt. Samia.

“Ni muhimu sana ofisi ya msajili wa hazina ihakikishe inasimamia ipasavyo sheria na kanuni zilizopo katika kuhakikisha kuwa taasisi za umma zinajiendesha kwa tija na kuipunguzia serikali mzigo wa gharama za kuziendesha,” alisema Rais Samia.

Pamoja na kutoa pongezi kwa Benki ya NMB, Rais Samia pia amemkabidhi cheti cha mlipa gawio kubwa serikalini katika sekta ya kibenki, Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo ya fedha Ruth Zaipuna.

Benki ya NMB imetoa gawio la shilingi Billioni 45.5 serikalini katika mwaka wa fedha uliopita.

Kwa mujibu wa Msajili wa Hazina, Nehemiah Kyando Mchechu, Serikali inamiliki asilimia 31.8 ya hisa katika benki ya NMB.

“Tumetoa tuzo kwa taasisi zilizofanya vizuri ili kuleta changamoto katika kujifunza sisi sote na ili taasisi zingine ziwe na wivu wa kusonga mbele ndio tuweze kuisaidia nchi yetu,” alisema Mchechu.

Kwa mujibu wa Msajili huyo wa Hazina, serikali imewekeza zaidi ya shilingi trillioni 73 katika taasisi za umma na kwamba ni jukumu lao kuhakikisha fedha hizo zinazaa matunda makubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

“Tunatarajia kuwa siku za mbeleni pamoja na kuwa na list of fame (orodha ya sifa), ya taasisi zinazofanya vizuri, baadae pia tungeweza kuwa na list of shame (ordha ya aibu) kwa taasisi zinazofanya vibaya lakini hatutarajii kufika huko, kutokana na maboresho makubwa tunayofanya kwa taasisi hizi kwa sasa,” alisema Mchechu.

Jumla ya taasisi 248 zimeshiriki mkutano huo wa kwanza wa mwaka wa kikao Kazi cha wenyekiti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma ukiwa na washiriki Zaidi ya 600.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.