• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia ashiriki mkutano wa UVIKO-19

Imewekwa tarehe: May 19th, 2021

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwa njia ya mtandao mkutano wa Wakuu wa Nchi na Mashirika ya Kimataifa uliojadili namna ya kuokoa uchumi wa nchi za Afrika kufuatia madhara yaliyosababishwa na janga la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19) na kufanyikakwa Jijini Paris kwa wito wa Rais wa Ufaransa Mhe. Emmanuel Macron.

Mkutano huo umehudhuriwa na Marais wa nchi za Angola, Burkina Faso, DRC, Code d'Ivoire, Misri, Ethiopia, Ghana, Mali, Mauritania, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal, Sudan, Togo, Tunisia, Italia, Hispania na Umoja wa Ulaya wakati Tanzania, Kenya, Afrika Kusini, Uholanzi, Ujerumani, China na Japan zimwshiriki kwa njia ya mtandao.

Mashirika ya Kimataifa yaliyoshiriki ni Umoja wa Mataifa (UN), Shirika la Fedha Duniani (IMF), Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo Duniani (OECD), Shirika la Biashara Duniani (WTO), Benki ya Dunia na mabenki mbalimbali.

Mhe. Rais Samia ameungana na Marais wengine Duniani kumpongeza Mhe. Rais Macron kwa kuitisha mkutano huo ambao wamesema umelenga sio tu kusaidia uchumi wa Bara la Afrika bali kuokoa maisha ya binadamu waliopo Afrika kutokana na kuathirika na madhara yaliyosababishwa na Korona.

Vile vile Mhe. Rais Samia amesema Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine duniani imekumbwa na madhara ya ugonjwa wa Korona ambayo yameathiri biashara, utoaji wa huduma za kijamii, kushuka kwa mapato, kupoteza maisha na kupoteza ajira mambo ambayo yamewaadhiri zaidi wanawake, vijana na watoto.

Aidha, amebainisha kuwa kutokana na athri hizo, Tanzania ambayo hivi karibuni imeingia katika uchumi wa kipato cha kati imechukua hatua mbalimbali ili kulinda uchumi wake na hasa miradi mikubwa ya kimkakati inayoitekeleza zikiwemo kuimarisha zaidi mazingira ya kufanya biashara ili kuvutia uwekezaji zaidi nchini.

Mhe. Rais Samia ametoa wito kwa washiriki wa mkutano huo hususani Jumuiya ya Kimataifa kuchukua hatua stahiki kuokoa uchumi wa nchi za Afrika zikiwemo mashirika ya fedha ya kimataifa kuongeza mikopo yenye masharti nafuu kwa miradi ya maendeleo ya nchi za Afrika na kusaidia sekta binafsi katika Bara la Afrika kwa kuiwezesha kupata mikopo nafuu ili kukuza biashara hasa ndogo na za kati ambazo ndio nguzo muhimu ya uchumi.

Hatua nyingine ni kusamehe mikopo ama kuongeza muda wa ulipaji wa mikopo ambayo nchi za Afrika zinadaiwa na kuchangia fedha katika bajeti za nchi za Afrika kutokana na nchi hizo kushindwa kufikia malengo ya ukusanyaji wa mapatoya ndani.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.