• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia atoa shilingi Bilioni 50 za kununua mahindi

Imewekwa tarehe: September 10th, 2021

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa shilingi bilioni 50 ambazo zitatumika kununua mahindi kutoka kwa wakulima ili kuwanusuru na kudodora kwa bei ya zao hilo.

Mhe. Majliwa ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Septemba 10, 2021) Bungeni wakati akiahirisha mkutano wa nne wa Bunge la 12, Jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Novemba 2, mwaka huu.

“Jana tarehe 9 Septemba 2021, Bunge lako tukufu lilipokea hoja binafsi kutoka kwa Mheshimiwa Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo ambayo iliungwa mkono na Waheshimiwa Wabunge. Serikali imesikia kilio cha wakulima kupitia Waheshimiwa Wabunge. Tayari tumepata shilingi bilioni 50 na ununuzi utaanza Jumatatu, tarehe 13 Septemba, 2021,” amesema.

Akitaja hatua nyingine ambazo Serikali imechukula ili kunusuru bei ya zao hilo, Waziri Mkuu amesema awali Serikali ilitoa sh. bilioni 15 kuuwezesha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kununua mahindi maeneo mbalimbali nchini. Amesema pia, Serikali ilishatoa sh. bilioni 10 kwa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) ili kuongeza mtaji wa ununuzi wa mazao.

“Naiagiza Wizara ya Kilimo izisimamie kwa karibu NFRA na CPB ili zinunue mahindi ya wakulima pekee, tena watoke ndani ya nchi. Aidha, ongezeni vituo vya kununulia mahindi hadi wilayani na kwenye miji midogo,” amesema.

Akibainisha hatua zaidi zilizochukuliwa, Waziri Mkuu amesema Serikali imetafuta masoko ya mahindi kwa kukamilisha mikataba mipya ya ununuzi wa mahindi na nchi za Sudan ya Kusini, DRC na Zimbabwe kama njia ya kuhakikisha wakulima hao wanapata soko la mahindi waliyozalisha.

“Hatua nyingine tuliyochukua ni kufungua mipaka kwa kipindi cha miezi miwili kwa ajili ya masoko ya nje ya nchi ambapo vibali vya usafirishaji hutolewa bure kupitia Ofisi za Wakuu wa Wilaya na kwa njia ya mtandao ili wafanyabiashara waweze kuvipata kwa urahisi. Upelekaji wa chakula utafanywa kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na hifadhi ya kutosha ya chakula,” amesisitiza.

Amezitaja hatua nyingine kuwa ni kuwaunganisha wafanyabiashara wa nafaka hapa nchini na wafanyabiashara wa nje kupitia Balozi za Tanzania na kuongeza thamani ya mazao.

Mbali na ununuzi wa nafaka, Waziri Mkuu amesema Serikali inafuatilia mwenendo wa upatikanaji wa mbolea ili kuhakikisha bidhaa hiyo inapatikana kwa wingi na kwa bei nafuu. “Lengo la Serikali ni kuwawezesha wakulima kumudu gharama za mbolea,” ameongeza.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametoa rai kwa wakulima na wanunuzi wa mazao waendelee kuuimarisha mfumo wa stakabadhi ghalani kwa vile umeonesha matokeo makubwa yenye manufaa.

“Mfumo wa stakabadhi ghalani ndiyo pekee uliothibitika na kuonesha matokeo makubwa yenye manufaa. Hivyo basi, tuendelee kuuimarisha katika mazao yote ya biashara nchini ili kuleta mafanikio kwa wakulima na Taifa kwa ujumla.”

Amesema Serikali imeondoa mifumo isiyo rasmi ya ununuzi wa mazao ambayo imekuwa ikiwakandamiza wakulima na kuwanufaisha baadhi ya wanunuzi wasiokuwa waaminifu. “Tuliondoa mifumo kama vile kangomba, butula, chomachoma, kula maua, njemke na mingineyo ambayo ilikuwa ikimpunja na kumnyonya mkulima.”

Ameyataja baadhi ya mazao yaliyonufaika na mfumo huo kuwa ni korosho, ufuta, dengu, choroko na kakao na kuongeza kuwa ufanisi wa mfumo huo, umekuwa kichocheo katika kupunguza umaskini na kuongeza uchumi wa nchi na wakulima.

“Taarifa zinaonesha kuwa kuuza mazao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na ushirika kunatoa nguvu ya pamoja kwa wakulima ya upatikanaji wa soko sambamba na kuimarisha bei ya mazao. Minada iliyofanyika imesaidia kuongezeka kwa bei ya mazao yaliyotumia mfumo wa stakabadhi ghalani ikiwemo korosho, ufuta, dengu, choroko na kakao.

“Mwaka 2020, bei ya choroko iliongezeka kutoka shilingi 600 hadi 800 kwa kilo na kufikia shilingi 900 hadi 1,300 kwa kilo katika vituo vya Magu, Uzogele, Igunga na Manyoni. Hivi karibuni tumeona bei ya kakao ikiongezeka maradufu kutoka shilingi 2,500 hadi 5,000 kwa kilo baada ya kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani.”

Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Kilimo ifanye kazi kwa karibu na vyama vya ushirika na vyama vya msingi kuhakikisha wanawawezesha wakulima kupata elimu na manufaa ya kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani bila usumbufu ili uwapatie tija.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.