• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Dodoma atamani Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ufanikiwe kwa 100%

Imewekwa tarehe: October 6th, 2024

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

MKOA wa Dodoma unatamani kuona zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa linafanikiwa kwa asilimia mia moja kwa kuhakikisha kila mwananchi anashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri wakati akifungua Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa lililofanyika katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma.

Alhaj Shekimweri alisema “Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma anatufundisha kujitambua na kujithamini kupitia kaulimbiu yake isemayo ‘Dodoma Fahari ya Watanzania’. Pia Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza miradi mkubwa katika Dodoma ikiwemo ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa kimataifa Msalato. Ujenzi wa Barabara ya Mzunguko na ujenzi wa Treni ya Kisasa ya Mwendo kasi SGR ambayo stesheni ya Dodoma ndiyo kubwa ikiwa na uwezo wa kupokea watu 2,500 kwa mara moja”.

“Kwa uzito huo ni lazima muamko wetu wakazi wa Dodoma kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uwe mkubwa sana. Tumuunge mkono mkuu wetu wa mkoa kwa kuhakikisha habaki hata mtu mmoja bila kuandikishwa ili malengo yetu tusishuke chini ya asilimia 100”.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi kufungua bonanza hilo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yamekamilika. Vifaa vyote vinavyohitajika vimefika na upande wa rasilimali fedha, Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewezesha kwa asilimia 100, aliongeza.

Bonanza la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 lilitanguliwa na ‘jogging’ iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma pamoja na watumishi wa umma kwa kupita katikati ya Jiji la Dodoma kuelekea Shule ya Sekondari Dodoma chini ya kaulimbiu isemayo “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi”.

MWISHO





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.