• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mtaka aahidi makubwa kwa wazee

Imewekwa tarehe: June 30th, 2021

Na Noelina Kimolo, DODOMA

SERIKALI mkoani Dodoma imewahakikishia wazee kuwa itaendelea kusimamia sera ya wazee kwa lengo la kuwahakikishia upatikanaji wa huduma bora kwa ustawi wa maisha yao kutokana na mchango wao mkubwa katika uchumi wa Tanzania.

Hakikisho hilo lilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Khamis Mkanachi alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka, katika hafla fupi ya uzinduzi wa Baraza la Wazee la Mkoa huo lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mkanachi alisema kuwa serikali kupitia Sera ya Taifa ya Wazee ya mwaka 2003 imeeleza kuwa wazee ni kundi muhimu katika jamii na wanapaswa kutambuliwa na kupewa fursa ya kushiriki katika mambo yanayohusu maisha ya kila siku kwa manufaa ya watanzania wote. Vilevile, inahakikisha wazee wanapata huduma zote muhimu ambazo zitawawezesha kushiriki kwa ukamilifu katika maisha ya kila siku.

“Serikali inaendelea kuwahudumia wazee katika upande wa afya, lishe na huduma zote za msingi ili kukidhi mahitaji ya mwanadamu huu ni wajibu wa msingi ambao serikali yetu imeuchukua” alisema Mkanachi.

Akiongelea uongozi wa baraza la wazee uliochaguliwa, alisema kuwa unawajibu wa kuwasaidia na kuwatetea wazee ili waweze kusimamia haki na ustawi katika kupewa kipaumbele kwenye huduma mbalimbali.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Nathalis Linuma alisema kuwa anatambua msaada utolewao na wazee kwa kuwa hata viongozi wengi kabla ya kufanya maamuzi huwa wanawashirikisha wazee katika maamuzi yao.

“Na utamaduni huo umekuwa ukiendelea kila siku na ndio maana hata sisi tukaona ni muhimu kuwa na Baraza la Wazee katika kuleta maendeleo ya taifa’’ alisema Linuma.

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Dodoma, Mchungaji Petro Mpolo alisema kuwa ni muhimu kwa wazee kujua haki zao katika kufanya maamuzi ili kuleta maendeleo katika jamii.

“Sisi wazee tunayo mambo mengi ambayo serikali tunahitaji mtusaidie. Wazee waliochaguliwa kuanzia ngazi ya Kata hadi Mkoa hawajui kazi yao na mipaka hivyo, tumeomba kupewa semina za mabaraza ya wazee ili watambue wajibu wao katika kazi zao” alisema Mchungaji Mpolo.

Pia ameomba Halmashauli ziwe zinatenga bajeti za kuwawezesha wazee kutekeleza majukumu yao kuanzia ngazi za chini hadi juu.

 

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.