• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yajipanga kukuza vipaji nchini

Imewekwa tarehe: June 8th, 2021

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) ameelekeza ufundishaji wa somo la Michezouimarishwe kuanzia shule ya awali, msingi, sekondari na vyuo ili kujenga haliya kujiamini na kuwa mahiri kimwili na kiakili.

Mhe. Majaliwa ameyasema hayo leo wakatiakifungua mashindano ya michezo na taaluma yajulikanayo kama UMISSETA naUMITASHUMTA yaliyofanyika kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara.

Ameeleza michezo ni muhimu zaidi kwa makuzina maendeleo ya taaluma ya watoto na vijana na ina mchango mkubwa katikakuimarisha afya ya mwili na akili.

“Watafiti wamethibitisha kuwa michezo kwamadarasa ya awali kwa maana ya miaka 3 – 6 ni muhimu zaidi katika kuongezauwezo wa mzunguko wa damu katika ubongo (kuongezeka kwa mishipa ya damu) namaendeleo ya afya na makuzi ya watoto kwa ujumla wake hivyo ni vyema tukajikitakumjenga mtoto huyu kuanzia kwenye ngazi ya awali;

Bila shaka sote tunaelewa kuwa binadamuhawezi kuwa na akili bora kwenye mwili dhaifu na afya bora inaweza kujengwavizuri zaidi kwa kushiriki katika michezo hivyo tujikite katika kutengenezavizazi vitakavyokua mahiri kwenye michezo wakati wote maisha yao.” Amesema Mhe.Majaliwa kwa msisitizo.

Majaliwa alibainisha kuwa katika siku za hivikaribuni kumekuwepo na mafanikio makubwa ya vijana waliyoyapata kupitia michezona wengi ni wa hapa hapa Tanzania, kama vile Mbwana Samata.

“Kwa hawa wachache wanatuonyesha picha kubwaya namna ambavyo vijana wetu wengi wanaweza kufanikiwa kupitia michezo na sanaatuongeze nguvu katika eneo hili,” amesema Majaliwa.

Aidha amesema Michezo na Sanaa vikiwekewamipango sahihi vina nafasi kubwa ya kuchangia na kujenga uchumi endelevu waTaifa na watu wake.

“Sekta hizi ni fursa kubwa kwa vijana wetukujiajiri, kuajirika na kuutambulisha utamaduni wetu ndani na nje ya mipaka yanchi yetu,” amefafanua zaidi Waziri Mkuu.

Hivyo basi, amewataka wanafunzi wotewanaoshiriki katika mashindano hayo kutoridhika na hatua waliyofikia kwenyemashindano hayo bali yawe mwanzo wa kujiimarisha katika michezo na sanaa ilikulitangaza Taifa kupitia michezo na sanaa.

Vile vile, amewakumbusha washiriki wa mashindanihayo amesema “Matarajio ya wengi ni kuona mkionyesha uwezo wenu kwa nidhamu yahali ya juu na kuiletea mafanikio mikoa yenu na taifa kwa jumla,” 

Waziri Mkuu pia amezitaka Wizara zinazohusikakurudisha mafunzo ya michezo katika vyuo vya Butimba na Mtwara ili kufundishawalimu watakaoweza kuwapa wanafunzi mafunzo sahihi ya michezo.

Kwa upande wake, Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa, amesema wanakusudia kuanzisha Vituovya kulea vipaji katika shule mbalimbali ili kuhakikisha kuwa vipaji vya watotovinaendelezwa kuanzia umri mdogo.

Naye, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Davidi Silinde ameelezea malengo ya mashindano hayo kuwa ni kujenga umoja wakitaifa, mshikamano na upendo baina ya wanafunzi wangali katika umri mdogo, kuimarishataaluma ya michezo kwa wanafunzi ili kuwajengea ujuzi na maarifa na kuwa mahiriwanapoendelea kukua pamoja na kujenga umoja, uzalendo na mshikamano miongonimwa wanafunzi, walimu na wadau wa michezo nchini.

Pia ameongeza kuwa mashindano hayoyatawajengea watoto ukakamavu na umahiri katika michezo pamoja na kuibua nakuendeleza vipaji vya wanafunzi wangali bado wachanga na kujenga dhana yauvumilivu na ustahimilivu.

Mashindano hayo yamebeba kauli mbiu ya “Michezo,Sanaa na Taaluma kwa maendeleo ya viwanda” na jumla ya wanamichezo 3,600 kutokamikoa 26 wanashiriki kwenye michezo ya UMITASHUMTA na wanamichezo 3,800 kutokakatika mikoa 28 ya Tanzania Bara na Visiwani wanashiriki katika michezo yaUMISSETA, mashindano hayo yatafungwa Julai 4, 2021.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.