• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hongera Lukundo Sekondari kwa kufuta daraja sifuri - Rweyemamu

Imewekwa tarehe: February 17th, 2023

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

AFISA Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu ameipongeza Shule ya Sekondari Lukundo kwa kufanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha Nne na kufuta daraja sifuri.

Mwalimu Rweyemamu alitoa pongezi hizo alipofanya ziara maalum katika Shule ya Sekondari Lukundo kwa ajili ya kuwapongeza walimu wa shule hiyo na kuwapatia zawadi.

Mwalimu Rweyemamu alisema “nilifurahi sana baada ya kuona matokeo yenu ya mtihani wa taifa wa kidato cha Nne mwaka 2022 Shule ya Sekondari Lukundo. Nilifurahi sana kuona hamna daraja sifuri hata moja, nilifurahi sana kuona ‘division’ I zilivyo nyingi, ‘division’ II zilivyo nyingi, ‘division’ III zilivyo nyingi. Asanteni sana.

Afisa elimu huyo aliitaja Shule ya Sekondari Lukundo kuwa ni mfano mzuri kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Mmethibitisha kwamba tunapoweka mikakati, tukashikamana tunatoka kwa mafanikio makubwa. Kwa hiyo, hakuna shule yoyote itakayosimama na kusema hatuwezi. Atakayesema hatuwezi nitamwambia nenda Shule ya Sekondari Lukundo ukajifunze” alisema Mwalimu Rweyemamu.

Mwalimu Rweyemamu aliitaka Shule ya Sekondari Lukundo kujipanga kufuta daraja la IV katika matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha Nne mwaka 2023. “Kama mmeweza kuondoa ziro mwaka 2022, inawezekana kabisa hata daraja la IV mkaliondoa katika matokeo ya mwaka 2023. Ninajua mnamipango mizuri na mikakati mizuri. Nataka kuwa natamba kuwa ninayo Shule ya Sekondari Lukundo inayofanya vizuri” alisisitiza Mwalimu Rweyemamu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Shule ya Sekondari Lukundo, Mwalimu Asafu Makonda alisema kuwa shule yake imefanikiwa kuondoa daraja sifuri kutokana na mshikamano uliopo. “Shule ya Sekondari Lukundo imeondoa daraja sifuri hapa Dodoma, Afisa Elimu Sekondari Jiji la Dodoma nikukumbushe tu kuwa hizi ni juhudi na mipango yako wewe mwenyewe. Utakumbuka baada ya matokeo ya moko mwaka 2022, ulikuja na program ya tokomeza ziro. Tuliona dhamira yako ya kufuta ziro na walimu wakatambua wakasema ngoja tupambane kwa mama huyu ambaye ameonesha upendo mkubwa” alisema Mwalimu Makonda.

Ikumbukwe kuwa shule ya sekondari Lukundo imefanikiwa kufuta daraja sifuri katika matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha Nne mwaka 2022, mwaka 2021 shule hiyo ilipata daraja sifuri tatu. Matokeo jumla yam waka 2022 daraja I (20), daraja II (47), daraja III (43) na daraja IV (116).

 


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.