• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali inadhamira ya dhati kuboresha sekta ya Habari

Imewekwa tarehe: December 17th, 2022

Na. Dotto Mwaibale, DAR ES SALAAM

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema Serikali inadhamira ya dhati ya kuboresha sekta ya habari nchini.

Nnauye ameyasema hayo wakati akifungua kongamano la maendeleoya ya sekta ya habari 2022 linaloendelea Ukumbi wa Mikiutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaaam.

Alisema serikali ina kila sababu ya kuboresha mazingira bora ya vyombo vya habari kutokana na umuhimu wake hasa katika maendeleo na kuinua uchumi wa nchi.

Nnauye alisema kuwa mwaka ujao wa 2023 Serikali imekusudia kuongeza nguvu zaidi katika kuboresha maslahi ya wanahabari ikiwa ni pamoja na kusimamia mikataba ya ajira zao na kulipwa madeni yao kutoka taasisi mbalimbali zikiwemo halmashauri za wilaya.

Katika hatua nyingine Nnauye amevitaka vyombo vya habari kutimiza wajibu kwa kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili na kulinda lasirimali za nchi na pale zinapotumika vibaya waendelee kuwafichua wabadhirifu.

Aliwaomba waandishi wa habari kuendelea kushirikiana na Serikali katika shughuli mbalimbali ili kuliletea taifa maendeleo na kukuza uchumi wa nchi na kueleza kuwa kongamano hilolitakuwa endelevu ambapo alipendekeza liitwe kongamano la kimataifa la maendeleo ya sekta ya habari badala ya kongomano la maendeleo ya sekta ya habari.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri wa Habari Tanzania (TEF) akizungumzia changangomo kadhaa zinazowakabili waandishi wa habari sambamba na madeni wanayodai alisema bado kunachangamoto kubwa ya ulipwaji wa madeni hayo.

“Mpaka sasa madeni ambayo vyombo vya habari vinadai kwa serikali na taasisi zake zikiwepo halmashauri ni zaidi ya Sh. 7 bilioni na ukijumlisha na deni la Gazeti la Daily News la serikali inakuwa Sh. 11 Bilioni hivyo kulifanya deni lote kufikia Sh. 18 Bilioni,” alisema Balile.

Katika kongamano hilo Wazri Nape alipata fursa ya kutoa tuzo kwa waandishi wa babari 10 na taasisi za serikali 10 waliofanya vizuri katika utoaji wa habari na kuandika habari na makala kwenye taasisi hizo ambapo Wizara ya Madini imetoa tuzo kwa baadhi ya waandishi.

Waandishi waliotunukiwa tuzo hizo ni pamoja na Nelly Mtema (Daily News), George Binagi (BMG Media) na Mohammed Zengwa (Global TV).

Kongamano hilo la siku moja linakutanisha wadau wa habari ikiwa ni pamoja na wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari, jukwaa la wahariri wa habari, maafisa habari kutoka Serikalini, Taasisi Binafsi na Mashirika ya Kimataifa.

Aidha, pia katika kongamano hilo zilitolewa mada mbalimbali kutoka kwa Dk. Rose Reuben kutoka TAMWA, Muadhiri wa Dipromasia Deus Kibamba, Kajubi Mkajanga kutoka Baraza la Habari Tanzania (MCT) Heliet Shija kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mkurugenzi Msaidizi wa Idara Habari (MAELEZO) Rodney Tadeus na Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayoub Ryioba.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.