• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali 'yamwaga' ajira 9,675

Imewekwa tarehe: May 10th, 2021

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu ametangaza nafasi za ajira za walimu 6,949 wa Shule za Msingi na Sekondari zinazolenga kujaza nafasi wazi za watumishi waliokoma utumishi wao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vifo, kuacha kazi, kufukuzwa kwenye utumishi na kustaafu.

Waziri Ummy alitoa kauli hiyo leo Mei 9, 2021 wakati alipofanya mkutano na waandishi wa habari katika ofisi za TAMISEMI jijini Dodoma kwa lengo la kutoa taarifa ya ofisi yake kupata kibali cha ajira kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

 “Tumepata kibali cha ajira za walimu 6,949 pamoja na watumishi 2,726 wa Kada ya Afya. Hivyo, nachukua fursa hii kuutangazia umma kuwa taratibu za kuanza mchakato wa kuomba ajira hizo umekamilika na kwamba waombaji wote wenye nia ya kuomba, sasa wanaweza kufanya hivyo”, alisema.

Alifafanua kuwa waombaji wanatakiwa kutuma maombi yao kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi ajira.tamisemi.go.tz kuanzia Mei 09 hadi 23 mwaka huu.

Hata hivyo, alieleza kuwa kwa upande wa watu wenye ulemavu hawatalazimika kutuma maombi yao kwa njia ya mtandao badala yake watatuma maombi yao yakiwa katika nakala ngumu.

“Kwa ndugu zetu wenye ulemavu wanaweza kutuma maombi yao kwa nakala ngumu. Maombi hayo yaeleze aina ya ulemavu na yaambatane na picha kisha yatumwe kwa Katibu Mkuu TAMISEMI. Nakala ya Maombi hayo itumwe Ofisi ya Waziri Mkuu ili Mkurugenzi wa Kitengo cha Watu wenye Ulemavu aione.

Waziri Ummy alisema Ofisi yake imebainisha sifa mbalimbali za kitaaluma ambazo waombaji wanapaswa kuwa nazo kulingana na muundo wa kada ya ualimu wa shule za msingi na sekondari nchini.

Akianza kueleza sifa za zinazotakiwa kwa walimu wa shule za msingizi, Waziri Ummy alisema katika nafasi ya Mwalimu Daraja IIIA, mwombaji anatakiwa kuwa mhitimu wa Astashahada ya Ualimu Elimu ya Msingi, Astashahada ya Ualimu Elimu ya Michezo, Astashahada ya Ualimu Elimu ya Awali na Astashahada ya Ualimu wa Elimu Maalum.

Aliongeza kuwa mwalimu Daraja la IIIB anatakiwa mhitimu mwenye Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Awali, Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Msingi na Stashahada ya Ualimu wa Elimu Maalum.

Vilevile, alisema kuwa katika nafasi ya Mwalimu Daraja la IIIC anatakiwa mhitimu mwenye Shahada ya Ualimu katika masomo ya “English Language, History na Geography”.

Kwa Upande wa shule za sekondari, Ummy alifafanua kuwa nafasi ya Mwalimu Daraja la IIIB inahitaji mhitimu wa Stashahada ya Ualimu wa masomo ya “Physics, Mathematics, Biology na Chemistry”.

Pia, katika nafasi ya Mwalimu Daraja la IIIC mwombaji anatakiwa kuwa na sifa mojawapo kati ya Shahada ya Ualimu, Shahada ya Elimu Maalum na Stashahada ya Uzamili katika Elimu (Post Graduate Diploma in Education) katika masomo ya “Physics, Chemistry, Biology na Mathematics”.

Waziri ummy aliongeza kuwa kwa waombaji waliopata elimu Nje ya Nchi, wanatakiwa kuzingatia taratibu zilizowekwa za kupata uthibitisho wa elimu zao kwa mamlaka zinazohusika kabla ya kuomba ajira hizo.

“Waombaji wote waliosoma Elimu ya Sekondari Nje ya Nchi wanatakiwa kupata namba ya ulinganifu wa matokeo kutoka Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA). Waombaji waliosoma Vyuo Nje ya Nchi wanatakiwa kupata Ithibati ya masomo yao kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).

Ummy alisisitiza kuwa kila mwombaji ni lazima awe Raia wa Tanzania mwenye umri usiozidi miaka 45, awe na namba ya kitambulisho cha Taifa, awe na vyeti kamili vya mafuzo ya fani aliyosomea na asiwe mwajiriwa wa Serikali au aliyewahi kuajiriwa na Serikali.

Mkutano huo wa Waziri na Waandishi wa Habari ulihudhuriwa na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama ambaye Ofisi yake ndiyo Mamlaka ya Ajira na Nidhamu kwa walimu wa shule za masingi na sekondari walioajiriwa katika utumishi wa Umma.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.