• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Tanzania kinara usambazaji umeme Afrika

Imewekwa tarehe: August 18th, 2020

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Tanzania imeshika nafasi ya kwanza barani Afrika kwa kusambaza umeme nchini kote kwa asilimia 80.

Alitoa kauli hiyo jana jijini Dar  es Salaam wakati akielezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano kwenye mkutano wa viongozi wa dini kutoka kamati za amani za mikoa Tanzania bara na Zanzibar.

"Leo hii Tanzania ni ya kwanza barani Afrika kwa kusambaza umeme kote nchini hadi vijijini na kufikisha asilimia 80. Kuna nchi ngapi barani Afrika, lakini Tanzania imefanikiwa kuwa ya kwanza. Tumeweza kufikia vijiji 9,112 Tanzania na hadi Aprili 2020 na tumetumia shilingi trilioni 2.27," alisema Majaliwa.

Mkutano huo uliandaliwa kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli na Serikali ya Awamu ya Tano katika ustawi wa amani, uzalendo na kumtanguliza Mungu.

Majaliwa alisema, ushirikiano mkubwa wanauonesha viongozi wa dini kwa Serikali, umewezesha kufanyika mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za upatikanaji wa nishati kwa ajili ya ustawi wa Watanzania.

Mbali ya upatikanaji wa umeme nchini, Waziri Mkuu alieleza mambo mengine 15 yaliyofanyika kwa ufanisi chini ya uongozi wa Rais Magufuli ikiwa ni pamoja na kurejesha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma; mapambano dhidi ya dawa za kulevya; ulinzi wa rasilimali za taifa; kuimarika kwa ukusanyaji mapato na kukua kwa uchumi.

"Tunao uwezo wa kuhimili ujenzi wa viwanda vipya na nipende kuwahakikishia wenye mitaji kwamba Tanzania ni mahali salama pa kuwekeza. Tulianza na mazao matano ya kimkakati lakini sasa tumeyaongeza. Kupitia kilimo tunazalisha mazao ambayo ni malighafi kwa viwanda vyetu," alisema Majaliwa.

Alitaja mafanikio mengine kuwa ni mapambano dhidi ya umasikini na ukosefu wa ajira; ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya afya; maboresho ya elimu; huduma za maji; ujenzi wa bwawa la kufua umeme la Nyerere, ujenzi wa mradi wa reli kwa kiwango cha kimataifa (SGR); usafiri wa anga; ujenzi wa meli na bandari na ujenzi wa barabara na madaraja.

"Suala la ajira ni kilio cha wote lakini kila nchi inatumia njia yake kukabliana nayo. Je tusingekuwa na miradi ya kimkakati kama SGR na Stieglers' Gorge, hawa watu milioni sita na zaidi wangekuwa wapi kwa sasa?"alihoji Waziri Mkuu.

Alisema, kupitia sekta za viwanda, kilimo, biashara, madini, utalii, miundombinu ya kimkakati na mifumo ya mikopo nafuu, Serikali imezalisha ajira za kutosha kwa Watanzania.

"Kupitia ujenzi wa viwanda vipya,tumetengeneza jumla ya ajira zipatazo 482,601 na kupitia utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya SGR, Stieglers' Gorge, ujenzi wa shule, hospitali na ufufuaji wa mashirika yetu tumefanikiwa kutengeneza ajira zipatazo 6,032,299."

Mapema, akitoa wasilisho la viongozi wa dini, Katibu wa Kamati ya Amani, Askofu Jackson Sosthenes alisema lengo la mkutano huo ni kumpongeza Rais Magufuli kwa hatua iliyofikiwa ya kuwa na uchumi wa kati kabla ya mwaka 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Amani, Sheikh Alhad Mussa Salum alisema ujasiri wa Rais Magufuli wa kutozuia ibada na kukataa kufungia watu ndani ulimpendeza Mwenyezi Mungu na akaamua kuifanya Tanzania kuwa nyota inayong'ara ulimwenguni.

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeiry ambaye alikuwa wa kwanza kutoa salamu za viongozi wakuu wa dini, alisema mtu mwenye akili anahitaji pointi ndogo tu kuona kinachofanywa na Rais Magufuli.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dk Alex Malasusa alisema amani ni msingi wa maendeleo yote.

"Viashiria vya ukosefu wa amani hatuvipendi, na tunaviombea vitoweke katika jina la Mungu…sisi viongozi wa dini tutaendelea kuiombea nchi yetu. Mungu anaipenda sana Tanzania, na hata tulipopita kwenye bonde la uvuli wa mauti la COVID 19, bado alituvusha. Tuendelee kumheshimu Mungu, kumtii na tuendelee kumwabudu Mungu," alisema.

Akizungumza kwa niaba ya Mufti wa Zanzibar, Sheikh Nooman Jongo alisema zamani Tanzania iliathiriwa mambo matatu ya udini, ukabila na uchama lakini kwa sasa hayapo.

Askofu Michael Hafidhi wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Zanzibar aliwataka viongozi wa vyama vya siasa waache kuwasema wenzao vibaya na kutumia majina ya maaskofu na masheikh kwa manufaa yao.


Chanzo: HabariLeo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.