• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TBC yazindua redio kwa mikoa kanda kati

Imewekwa tarehe: July 26th, 2021

WAZIRI wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Dkt.Faustine Ndugulile,amezindua studio za TBC Redio Jamii Kanda ya Kati ambazo zimefadhiliwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa kushirikiana na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC).

Akizungumza  leo Julai 26,2021 jijini Dodoma mara baada ya uzinduzi huo Waziri Ndugulile,amesema kuwa  lengo la kuzindua studio hizo ni kuboresha usikivu wa Radio Kanda ya Kati.

”Niwapongeze UCSAF na TBC kwa ushirikiano wenu huu wa kuanzisha Redio Jamii ambayo sasa itakuwa na manufaa kwa wananchi wa Mikoa ya Kanda ya Kati, niwahakikishie kama Wizara tutaendelea kushirikiana nanyi katika kuleta usikivu wa mawasiliano,” Amesema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt.Ndugulile amesema kuwa Serikali imetangaza zabuni ya leseni na masafa na kuwa tayari imetenga shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya kuboresha usikivu.

“Tayari tumeshatangaza zabuni ya leseni na masafa katika maeneo ambayo hayana usikivu wa redio, tunawaombea Wananchi wenye nia ya kuwekeza watumie fursa hiyo,” amesema.

Aidha, Dkt. Ndugulile amesema serikali pia itafanya mapitio ya tozo za Redio kwenye Wilaya na maeneo ya mipakani ambapo itapunguza tozo hizo kwa lengo la kuongeza usikivu kwenye wilaya hizo.

Pia Dkt. Ndugulile ametoa wito kwa watanzania kufika kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano TCRA ili kuangalia Wilaya ambazo tenda hizo zimetangazwa ambapo zitaenda sambamba na punguzo la leseni kwenye Redio hizo.

Kwa upande wake Naibu waziri, Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Pauline Gekul, amesema kuanzishwa kwa redio hiyo ni jambo la kihistoria kutokana na uhumimu wake kwa Taifa hasa katika kufikisha huduma za matangazo ya redio kwa wananchi wa Makao Makuu na mikoa ya jirani.

“Kituo hiki kimefunguliwa leo tunategemea masuala ya kawaida yanayowagusa watanzania yanakwenda kuzungumzwa na burudani mbalimbali zinaenda kutolewa pamoja na vipindi vinavyokwenda kurushwa ni vya utalii, kilimo na ufugaji, michezo, vijana, muziki, mila na desturi,” amesema Waziri Gekul.

Aidha, ametoa wito kwa vyombo vya habari nchini kuzingatia weledi na kuhakikisha maudhui yanayokwenda kwa wananchi hayapotoshi na ni sahihi na kweli.

Awali Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano Kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba amesema gharama halisi ya ukarabati na ununuzi wa vifaa vya Radio Jamii hiyo ni Shilingi Bilioni 1.71 huku TBC wenyewe wakichangia Shilingi Milioni 163.

Mashiba amesema uzinduzi wa Radio hiyo ni muendelezo wa Mfuko huo kurahisisha mawasiliano ambapo awali walishafanya hivyo jijini Arusha na leo ni zamu ya Dodoma.

”Tarehe 30 tutazindua kituo kingine cha kurusha matangazo katika eneo la Kisaki ambacho pia tumekifadhili sisi lengo ni kuhakikisha Radio yetu ya Taifa inasikika kila kona.

“Sisi na  TBC tumeendelea kushirikiana kutekeleza miradi ya upanuzi wa usikuvu wa Mawasiliano wenye lengo la kupeleka huduma ya habari kwa wananchi kwa njia ya redio” amesema Mashiba.

Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayoub Rioba amesema kuwepo kwa Redio hiyo, kutasaidia katika kurusha habari za kikanda ili kukuza uelewa wa wananchi kuhusiana na masuala ya kijamii katika maeneo yao.

”Redio hii  itaongeza uwezo wa kuandaa vipindi vinavyohusu matukio ya kitaifa ikiwemo vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kurusha vipindi vya runinga kutokea Dodoma ikiwemo vipindi vya Jambo Tanzania na TBC Aridhio” amesema Dkt.Rioba

Hata hivyo Dkt. Rioba ameishukuru UCSAF kwa ufadhili huo na kuwataka wananchi wa Dodoma na Mikoa jirani kuitumia Redio hiyo kama fursa ya kujikwamua kiuchumi, kielimu na kijamii.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.