• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba, 2024

Imewekwa tarehe: August 16th, 2024

Na. Anna Stanley, DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamedi Mchengerwa ametoa tangazo la uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka na uchaguzi utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

Mchengerwa aliyasema hayo katika viwanja vya Chinangali park, jijini Dodoma wakati akizungumza na wananchi na kuwahamasisha kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa na kujitokeza kupiga kura.

"Tangazo hili limetolewa chini ya Kanuni ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ya mwaka, 2024 pamoja na matangazo ya serikali Na. 571, Na. 572, Na. 573, Na. 574 ya mwaka 2024" alisema Mchengerwa.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 145 na Ibara ya 146, inaeleza uwepo wa Serikali za Mitaa pamoja na madhumuni yake ambapo miongoni mwa madhumuni ni pamoja na kupeleka madaraka kwa wananchi, alisema.

“Sheria za Serikali za Mitaa, Mamlaka za Wilaya, sura Na. 287 ya Serikali za Mitaa, Mamlaka kamili, sura Na. 288 zinaelekeza kufanyika kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, lengo ni kufanya serikali za mitaa ziongoze kidemokrasia. Kwa mujibu wa kifungu cha 201 ‘A’ cha Sheria za Serikali za Mitaa Mamlaka za Wilaya, sura Na. 287 na kifungu Na. 77A, huongoza uchaguzi huo wa serikali za mitaa, na viongozi wanaochaguliwa katika ngazi hii ni, wenyeviti wa vijiji, wajumbe wa halmashauri ya vijiji, wenyeviti wa mitaa, wajumbe wa kamati za mitaa na wenyeviti wa vitongoji, wagombea wote katika ngazi mbalimbali za uongozi wanatakiwa kuwa wanachama wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu" alisema Mchengerwa.

Uchaguzi wa mwisho wa serikali za mitaa ulifanyika mwezi Novemba, 2019. Hivyo, uchaguzi mwingine unatakiwa kufanyika mwezi Novemba, 2024, uandikishaji na uandaaji wa orodha ya wapiga kura utaanza siku 47 kabla ya tukio la uchaguzi, aliongeza.

Kwa tangazo hilo, wananchi wote wanaobwa kujitokeza kwa ajili ya kujiandikisha kupiga kura, kugombea na kushiriki katika uchaguzi huo ili kupata viongozi wa serikali za mitaa kwa maendeleo ya nchi wakati kampeni zitaanza tarehe 20–26 Novemba, 2024 na uchaguzi utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

MWISHO.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.