• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ujenzi nyumba 1,000 Dodoma, Majaliwa aweka jiwe la msingi

Imewekwa tarehe: October 31st, 2021

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amesema Serikaliya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan itaendeleakuuboresha Mji wa Dodoma kwa kujenga miundombinu ya barabara, maji pamoja nanyumba za watumishi.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo Jumapili, Oktoba 31, 2021 baada ya kuweka jiwela msingi la ujenzi wa nyumba 1,000 za makazi zinazojengwa na Shirika la Nyumbala Taifa (NHC) katika eneo la Chamwino na Iyumbu Mkoani Dodoma.

Akifafanua zaidi amesema kuwa hivi karibuni Rais Samiaametoa shilingi Bilioni 20 ambazo ni mkopo nafuu kwa Shirika la Nyumba la Taifaili ziwe mtaji wa kujenga nyumba 1,000 katika maeneo ya Chamwino na Iyumbujijini Dodoma ambao hadi kukamilika kwake mradi huo utagharimu Shilingi Bilioni71 huku awamu ya kwanza ikitumia Bilioni 21.4 kukamilisha nyumba 404.

Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza kwenyemiradi mikubwa ya ujenzi wa majengo ya Ofisi na Makazi kwa Watumishi wa Ummaili kupunguza gharama kubwa ya kodi ya pango pamoja na kuimarisha utendaji nauwajibikaji wa watumishi hao katika kuwahudumia Watanzania.

Aidha, Waziri Mkuu ameliagiza Shirika la Nyumba la Taifakukaa pamoja na DUWASA, TARURA na TANESCO ili kuona namna bora ya kushirikianana kufanikisha upatikanaji wa miundombinu hiyo muhimu na kupunguza mzigo wagharama kwa Shirika hilo ili miradi hiyo iweze kukamilika kwa wakati na kwagharama nafuu.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema “Wakurugenzi wa Halmashaurihususan halmashauri mpya tumieni Shirika la Nyumba la Taifa pamoja na WatumishiHousing ili muweze kuharakisha ujenzi wa nyumba bora za watumishi waHalmashauri kwa gharama nafuu.”

Vilevile, Mheshimiwa Majaliwa ameliagiza Shirika hilokupunguza gharama za manunuzi kwa kununua vifaa kama mabati, mabomba, vigaekutoka kwa wazarishaji wa ndani ya nchi kwa kuweka oda maalum ili miradiikamilike kwa muda uliopangwa na kuhakikisha sheria na taratibu za manunuzizinafuatwa ipasavyo.

Awali, akizungumza baada ya kukagua ujenzi wa nyumba 100katika eneo la Chamwino, Waziri Mkuu aliipongeza Wizara ya Ardhi pamojana Shirika la Nyumba la Taifa kwa hatua ya ujenzi nyumba hizo pamoja nampango wa ujenzi wa nyumba za makazi.

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amewapongeza wafanyakaziwakitanzania walioshiriki katika ujenzi wa nyumba hizo ikiwa ni utekelezaji wamsisitizo wa Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu ushirikishwaji wa watanzaniakatika ujenzi wa miradi mikubwa ya ujenzi.

Naye Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi, amesema Serikali kupitia Shirika la Nyumba la Taifa haitaruhusuutaratibu wa mtu mmoja kununua nyumba nyingi katika eneo hilo na kisha kuanzautaratibu wa kupangisha, ila watatoa fursa sawa kwa Watanzania wa kada zote iliwaweze kunufaika na mradi huo.

Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Dkt. MaulidBanyani pamoja na kuishukuru Serikali kwa kutoa mkopo nafuu kwa Shirika hiloamesema awamu ya kwanza ya mradi wa nyumba 1,000 unaotekelezwa na Shirika hiloMkoani Dodoma ulianza Januari 6, 2021 kwa eneo la Iyumbu na Chamwino ulianzaFebruari 1, 2021.

“Mradi huu mkubwa unaohusisha ujenzi wa nyumba za makazi 1,000katika Jiji la Dodoma utagharimu Shilingi bilioni 71 hadi kukamilika ambapoawamu hii ya kwanza yenye nyumba 404 itagharimu shilingi bilioni 21.4 na kazikubwa ya ujenzi itakuwa imekamilika ifikapo Desemba 2021 na kubakiwa naukamilishaji wa kazi chache za nje ambazo nazo zitaisha mwezi Januari 2022.”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.