• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

VITENGO vya Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Dodoma vyapongezwa kwa kuhabarisha wananchi juu ya kazi nzuri zinazofanywa na serikali

Imewekwa tarehe: July 2nd, 2024

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

VITENGO vya Mawasiliano Serikalini katika Mkoa wa Dodoma vimepongezwa kwa kuhabarisha wananchi juu ya kazi nzuri zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya Mkoa wa Dodoma kushika nafasi ya nne katika utoaji habari nchini kufuatia tathimini iliyofanywa na Idara ya Habari (Maelezo) chini ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari juu ya umahili wa utoaji habari kwa vitengo vya mawasiliano serikalini.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Kaspar Mmuya wakati akipokea zawadi ya kikombe na cheti baada ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kushika nafasi ya nne kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara.

Mmuya alisema “napenda kuwapongeza kwa kazi nzuri ya kuhabarisha wananchi juu ya kazi na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Mkoa wa Dodoma. Hakika mmemuheshimisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mheshimiwa Rosemary Senyamule. Nimefahamishwa kuwa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kimeshika nafasi ya nne, Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Jiji la Dodoma kimeshika nafasi ya 13 na Halmashauri ya Mji wa Kondoa nafasi ya 15. Mwaka huu tulioanza tunataka kupiga hatua zaidi na kushika nafasi ya kwanza kwa sababu Dodoma ndiyo fahari ya watanzania”.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipambanua katika kukuza uhuru wa habari ili wananchi waweze kupata habari sahihi. Habari sahihi zinapatikana katika vitengo vya mawasiliano serikalini. “Nimefurahishwa na umahiri wenu katika kuuhabarisha umma, matumizi ya mitandao ya kijamii na uhuishaji wa tovuti za serikali. Wito wangu kwenu endeleeni kujipanga zaidi ili habari na taarifa sahihi ziwafikie wananchi wengi zaidi” alisema Mmuya.

Kwa upande wake Afisa Utumishi Mkuu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Lucy J. Timba, wakati akikabidhi zawadi ya kikombe na cheti kwa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, alisema kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na halmashauri zake mbili wamefanya vizuri katika tuzo za umahili wa vitengo vya mawasiliano serikalini kwa utoaji wa habari kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Alisema kuwa katika tuzo hizo Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kilishika nafasi ya nne na kupewa zawadi ya kombe na cheti cha utambuzi. “Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmasahuri ya Jiji la Dodoma kilishika nafasi ya 13 na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Mji Kondoa kilishika nafasi ya 15 na wote kupewa zawadi ya cheti cha utambuzi" alisema Timba.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Hellen Minja alisema kuwa kitengo chake kimejipanga kupiga hatua zaidi. “Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma tunampango wa kufanya vizuri zaidi na kuwa washindi namba moja katika kuhabarisha umma nchini. Tutafanya kazi zaidi ya mwanzo ili tuwe bora” alisema Minja.

Tuzo ya umahili wa vitengo vya mawasiliano serikalini vilivyofanya vizuri kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ilitangazwa na Mkurgenzi wa idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 18 June, 2024 katika Kongamano la pili la maendeleo ya sekta ya Habari nchini lililohudhuriwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na zawadi kukabidhiwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 21 June, 2024 katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.






Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.