• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waajiri Dodoma watakiwa kusaidia wanawake kunyonyesha kazini

Imewekwa tarehe: August 7th, 2023

Na. Dennis Gondwe Dodoma,

WAAJIRI katika Mkoa wa Dodoma wametakiwa kutoa msukumo katika kurahisisha na kusaidia wanawake walioajiriwa kuendelea kunyonyesha watoto wao kwa mujibu wa taratibu ili wawe na lishe bora.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika hotuba yake kwenye matembezi ya hiari kuhamasisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama na kusomwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri yaliyoishia uwanja wa Shule ya Msingi Chang’ombe jijini hapa.

Senyamule alisema kuwa lengo kuu la maadhimisho ya mwaka huu ni kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa kusaidia wanawake waweze kufanya kazi za uzalishaji pamoja na utunzaji wa watoto wao. Alisema kuwa ili kufanikiwa “lazima kuhamasisha na kutetea utekelezaji wa mikakati inayowezesha waajiri kuwa karibu na familia, walezi au mama wa mtoto na kutoa msukumo katika kurahisisha na kusaidia wanawake walioajiriwa kuendelea kunyonyesha watoto wao. Kuwahimiza waajiri kutenga sehemu maalum kwa ajili ya wafanyakazi wanawake wanaonyonyesha ili waendelee kufanya hivyo mahali pa kazi”.

Alisema kuwa maadhimisho hayo yanalenga kuelimisha umma kuhusu sheria ya kulinda haki za uzazi kwa wanawake na nyingine za kitaifa. “Vilevile, kuwawezesha wanawake kufanya kazi na kunyonyesha watoto wao ipasavyo kwa kushawishi upatikanaji wa aina mbalimbali za msaada kutoka kwa wadau katika sekta zote” alisema Senyamule.

Akioanisha majukumu ya uzalishaji mali, uzazi na maisha ya wanawake na wanaume kwa pamoja, alisema kuwa kutaleta faida kwenye sekta zote katika jamii. “Faida zinazopatikana ni pamoja na uboreshaji tija, kipato cha familia na usalama wa kazi, ustawi na afya ya wanawake na watoto, kufaidika kwa waajiri na kuwepo kwa taifa lenye mfumo imara wa kijamii na kiuchumi” alisema Senyamule.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mradi wa USAID/ Lishe Endelevu unaofadhiliwa na USAID na kutekelezwa na Shirika la Save the Children, Joyceline Kaganda alisema kuwa mchango wa mradi katika kufanikisha juhudi za serikali kuhusu afua ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama ikiambatana na ufanyaji kazi kwa ajili ya kujikimu. “Mradi umewezesha mafunzo na vitendea kazi ili kuimarisha lishe ya wanawake wajawazito, wanaonyonyesha, watoto wachanga, wadogo na vijana balehe kwa WAJA wapatao 4,000, Mkoa wa Dodoma peke yake walikuwa WAJA 1,221. Hawa wanatumika kumfikia mlengwa katika elimu ya unyonyeshaji moja kwa moja hadi ngazi ya kaya. Mradi pia ulitoa mafunzo ya unasihi wa lishe kwa watoa huduma wa afya 600 na kwa Mkoa wa Dodoma ni 220 wanaendelea kuimarisha uelewa wa walengwa kila wanapohudhuria kliniki kuanzia ujauzito na ufuatiliaji wa hali ya lishe ya mtoto” alisema Kaganda.

Fursa nyingine ya mradi aliitaja kuwa ni kutoa mafunzo ya mbinu bora za kilimo, mifugo, na uvuvi kwa maafisa ugani 800 kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa chakula mchanganyiko chenye virutubishi vingi katika ngazi ya kaya na kuongeza kipato cha kaya. “Sote tutakubaliana ili mama atengeneze maziwa ya kutosha ni lazima apate mlo wa kutosha na wenye mchanganyiko wa vyakula kutoka makundi yote ya vyakula. Pia awe na mahitaji mengine ya msingi ili kumpunguzia msongo wa mawazo” alisema Kaganda.

Nae Afisa Lisha wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Semeni Eva Juma alisema kuwa mama anayenyonyesha anatakiwa kupunguziwa kazi na msongo wa mawazo. “Siku 1,000 za mwanzo bora wa mtoto ndiyo maisha bora mtoto, ukikosea hapo mtoto anadumaa kiakili na uwezo wa kufikiria unadumaa. Hivyo, tunashauri maziwa ya mama mtoto aanze kunyonya ndani ya saa moja tangu anapozaliwa. Kipindi hiki ndiyo muda maziwa ya kwanza ya njano yanayokuwa na virutubishi vyote muhimu kwa lishe bora ya mtoto yanauhumu kwa mtoto. Baada ya hapo endelea kumnyonyesha mtoto kadri anavyohitaji” alisema Juma.

Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji tarehe 1-7 Agosti, 2023 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Saidia unyonyeshaji: Wezesha wazazi kulea watoto na kufanya kazi zao kila siku”.  


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.