• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wagonjwa 11 wafanyiwa upasuaji wa moyo bila ya kuusimamisha moyo JKCI

Imewekwa tarehe: April 14th, 2021

Wagonjwa 11 wamefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wa bila kuusimamisha moyo katika kambi maalum ya matibabu ya moyo inayofanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Subhash Sinha wa Hospitali ya MAX iliyopo New Delhi nchini India.

Kambi hii ya siku 10 ambayo inaenda sambamba na utoaji wa mafunzo na kubadilishana ujuzi kwa wataalamu wa upasuaji wa Taasisi yetu ilianza tarehe 10 na itamalizika tarehe 19 mwezi huu ambapo baadhi ya upasuaji unaofanyika ni ule ambao haufanyiki hapa nchini.

Upasuaji wa moyo unaofanyika katika kambi hii ni wa kupandikiza mishipa ya damu ya moyo (Coronary Artery Bypass Graft Surgery - CABG) kwa wagonjwa ambao uwezo wa moyo wao kufanya kazi umepungua kwa kiwango cha chini cha asilimia 35.

Upasuaji wa aina hii unafanyika katika Taasisi yetu, tofauti iliyopo ni kuwa wataalamu wetu walikuwa wanausimamisha moyo wakati wanafanya upasuaji lakini katika kambi hii upasuaji unafanyika huku moyo ukiendelea kufanya kazi kama kawaida. Wagonjwa saba wameshafanyiwa upasuaji huu hadi sasa. Kufanyika kwa upasuaji wa aina hii kutawasaidia wagonjwa kupona haraka na kukaa hospitali kwa siku chache.

Aidha upasuaji mwingine unaofanyika katika kambi hii ni kwa watu wenye matatizo ya mshipa mkubwa wa damu wa kifuani (Thoracic and Abdominal Aortic Aneurysm Dissection). Hadi sasa wagonjwa wanne wameshafanyiwa upasuaji wa aina hii.

Tunaamini kambi hii itawasaidia wataalamu wetu kupata ujuzi wa kutosha ambao utawasaidia kufanya upasuaji wa aina hii siku za karibuni.

Changamoto kubwa tunayokutana nayo ni upatikanaji wa damu kwani wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo wanahitaji kuongezewa damu nyingi kati ya chupa sita hadi saba. Tunawaomba wananchi muendelee kujitolea kuchangia damu kwa ajili ya wagonjwa kwa kufanya hivyo kutasaidia kuokoa maisha yao.

Hadi kumalizika kwa kambi hii tarehe 19/04/2021 tunatarajia wagonjwa 20 watakuwa wamefanyiwa upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu ya moyo na wagonjwa nane watakuwa wamefanyiwa upasuaji wa mshipa mkubwa wa damu wa kifuani. Wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wanaendelea vizuri na wengine wamesharuhusiwa kutoka katika chumba cha uangalizi maalum na kurudi wodini kwa ajili ya kuendelea na matibabu ikiwemo mazoezi.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Subhash Sinha kutoka hospitali ya Max iliyopo New Delhi nchini India akishirikiana na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kupandikiza mishipa ya damu ya moyo (Coronary Artery Bypass Graft Surgery - CABG) kwa wagonjwa bila ya kuusimamisha moyo katika kambi maalum ya siku 10 inayofanyika katika Taasisi hiyo.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Subhash Sinha kutoka Hospitali ya Max iliyopo New Delhi nchini India akiwafundisha wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) njia mbalimbali za kufanya upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu ya moyo (Coronary Artery Bypass Graft Surgery - CABG). Mafunzo hayo yanaenda sambamba na kambi maalum ya upasuaji wa moyo ya siku 10 inayofanyika katika Taasisi hiyo.

Baadhi ya wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia mafunzo ya upasuaji wa mshipa mkubwa wa damu wa kifuani (Thoracic and Abdominal Aortic Aneurysm Dissection) yaliyokuwa yanatolewa leo na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu Subhash Kumar Sinha kutoka Hospitali ya Max iliyopo New Delhi nchini India. Mafunzo hayo yanaenda sambamba na kambi maalum ya upasuaji wa moyo ya siku 10 inayofanyika katika Taasisi hiyo.Picha na JKCI.

Chanzo: issamichuzi.blogspot.com


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.